• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Halmashauri za Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na Meatu Mkoani Simiyu zimekubaliana kwa pamoja kufunga Ziwa Kitangiri ili kuboresha mazingira ya mazalia ya samaki

Posted on: January 12th, 2019


HATIMAYE Halmashauri za Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na Meatu Mkoani Simiyu zimekubaliana kwa pamoja kufunga Ziwa Kitangiri ili kuboresha mazingira ya mazalia ya samaki kwa manufaa ya Halmashauri hizo.

Makubaliano hayo yamefanyika juzi katika kikao cha pamoja cha Ujirani mwema kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Meatu Mkoani Simiyu ambapo Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya hizo wakiongozwa na Wakuu wa Wilaya hizo ambao ni Wenyeviti wa kamati za Ulinzi na usalama.

kikao hicho kiliwakilishwa na Simon Tyosela Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iramba, Pius Machungwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, kamati za Ulinzi na Usalma za Wilaya zote, Madiwani, pamoja na  wakuu wa Idara.

Akifungua kikao hicho cha Ujirani mwema Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dk. Joseph Chilongani alisema kuwa, imekuwa jambo zuri kwa kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Wenyeviti wa Halmashauri zote mbili na baadhi ya Madiwani wa Halmashauri kuwa na kikao cha pamoja cha kuhakikisha tunalinda Ziwa Kitangiri kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Halmashauri hizo.

‘’ Ni jukumu letu sisi viongozi wa Wilaya hizi kuhakikisha tunatunza na kuhifadhi mazingira ya Ziwa Kitangiri ili kutoa fursa samaki wazaliane kwa wingi na wakubwa kwa ajili ya kitoweo kwa jamii na kuwaongezea kipato wananchi kwa ujumla pamoja na kuongeza mapato ya Halmashauri zetu.’’

‘’ Cha msingi Halmashauri wilaya za Iramba Meatu, Igunga na Wilaya ya Kishapu tulikuwa na utaratibu wa pamoja za Kufunga Ziwa Kitangiri kila mwaka lakini hatukuwa mpango mkakati wa pamoja kuamua ni lini ziwa hili litakuwa linafungwa kila mwaka, hata hivyo katika kikao cha Ujirani mwema tuliofanya mjini Shinyanga mwaka juzi tulikubaliana kuhifadhi Ziwa Kitangiri na kupiga vita kwa nguvu uvuvi haramu na kuhakikisha mazingira ya Ziwa yanakua mazuri ili samaki wazaliane kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.’’ Alisisitiza Dkt. Chilongani

Alipokuwa Katika Kijiji cha Usulize Wilayani Meatu kwenye kambi ya wavuvi ya kijiji hicho alitangaza rasmi kufunga Ziwa hilo.

‘’ Mkuu wa Wilaya ya Iramba na Wenyeviti wa Halmshauri zote na kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya hizi leo hii natamka kuwa Ziwa Kitangiri limefungwa hadi tarehe 01 mwezi Aprili mwaka huu hivyo kuanzia tarehe 17/04/2019 ndiyo Ziwa litafunguliwa Rasmi na shughuli za uvuvi zitaanza tena na yeyote atakayekiuka atachukuliwa hatua za kisheria’’ alionya Mkuu huyo wa Wilaya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula alisema tayari kwa upande wa Wilaya ya Iramba Ziwa Kitangiri limeshafungwa toka tarehe 01 mwezi Januari na litafunguliwa tarehe 01 mwezi Aprili 2019

‘’ Ndugu Mkuu wa Wilaya ya Meatu kwa upande wetu tulikwisha funga Ziwa Kitangiri kama kawaida yetu ya kila mwaka isipokuwa mwaka huu tumeona tuje kujiriridhisha katika Wilaya ya Meatu maana miaka yote sisi tulikuwa tukifunga Ziwa upande wa Meatu wanavua hii ilikuwa inawatia unyonge sana wavuvi wa upande wa Iramba’’

‘’ Kwa hiyo hivi sasa tutahakikisha kwamba zuio la uvuvi liheshimiwe na ifikapo tarehe iliyopangwa mvuvi yeyote atakayeonekana katika kambi za uvuvi au Ziwani akivua samaki itakuwa halali yetu, hatutakubali watu wanaharibu mazalia ya samaki tukiwaangalia tu . hata Ziwa likifunguliwa ni marufuku kutumia nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu, itafanyika dori ya nguvu kuhakikisha Ziwa hili linalindwa kwa nguvu zote’’ alisistiza Mhe: Luhahula

Kikao hicho cha ujirani mwema kimewaeleza wataalamu wa Halmashauri za Wilaya za Meatu, Iramba, Kishapu na Igunga ambao wananchi wake wanaonufaika na Ziwa hilo watengeneze Rasimu na kuweka sheria ndogo ndogo za kulinda Ziwa hilo na wamepewa mwezi mmoja kuandaa rasimu hiyo ambayo itakuwa ndiyo dira ya kudhibiti Ziwa hilo lisihujumiwe.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.