• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

Posted on: September 22nd, 2023

MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla.

Ametoa kauli hiyo tarehe 22 Septemba, mwaka 2023 muda mfupi baada ya kumaliza kutembelea, kukagua, kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru ambao umepokelewa kutokea Mkoani Tabora.

Akiwahutubia wananchi wa kata ya Kiomboi, Tarafa ya Kisiriri Wilaya ya Iramba Mkoani Singida muda mfupi baada ya kumaliza kukagua miradi ya maendeleo, amesema kuwa miradi mingi inakwama kutokana na watekelezaji au wasimamizi wa miradi hiyo kutoa au kupokea rushwa kwa nia ya kukinufaisha wenyewe.

Amesema kuwa ili kuwa na miradi bora na yenye kukubalika ni lazima kila Mtanzania kuhakikisha anapinga na kupiga kelele juu ya kuzuia vitendo viovu ambavyo vinatokana na vitendo viovu vya utoaji au upokeaji wa rushwa na kusababisha miradi au huduma kuwa chini ya ubora.

"Tunasema kuwa tupambane na rushwa kwa maana kwamba unaweza kuona kuwa mtu akitoa rushwa au kupokea rushwa anaweza kufanya kazi chini ya kiwango na kusababisha huduma kuwa mbovu.

"Tatizo la rushwa bado lipo nchini na imefika wakati watanzania wanaweza kuichukia Serikali yao kwa kukosa huduma nzuri pale mmoja anapokuwa amepokea rushwa au kutoa rushwa kwani ni wazi kuwa rushwa upotosha haki" amesema mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Akizungumzia suala la amani Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge kitaifa amewataka watanzania kuwa mabalozi waaminifu katika kutunza amani ya nchi kwa kusimamia amani, upendo mshikamano pamoja na kuendeleza na kulinda umoja wa kitaifa.

Kuhusu utunzaji wa mazingira Abdalla amewataka watanzania kuhakikisha wanatunza mazingira ili kuepuka kupata magonjwa yanayosababishwa na uchafu na kuepukana na kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo yenye vyanzo vya maji.

Amesema kwa sasa kuna hali ya mabadiliko ya tabia nchi hivyo ni vyema kuhakikisha watanzania wote kwa ushirikiano wa wanatunza vyanzo vya maji na kukaa zaidi ya mita 60 zaidi ya chanzo cha maji.

Sambamba na hilo Abdalla amesema ili kulinda nguvu kazi ya taifa ambapo asilimia kubwa ni vijana kila mmoja awe askari kwa lengo la kupambana na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Amesema kuwa vijana wengi ndo nguvukazi ya taifa hivyo wanatakiwa kutokutumia dawa za kulevya huku akiwashauri watanzaia kujiepusha na uagizaji, usambazaji pamoja na kilimo ambacho ni halamu.

Mwisho.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.