• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU WA MKOA WA SINGIDA DKT. BINILITH MAHENGE ATEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA WILAYANI IRAMBA.

Posted on: November 30th, 2021

Wilaya ya Iramba mkoani Singida inatarajia kukabidhi jumla ya vyumba vya madarasa 61 ambavyo ni miradi ya elimu yenye thamani ya Sh. Bilioni 1.89 iliyojengwa kwa kutumia fedha za UVIKO 19 ifikapo tarehe Desemba 5, 2021.

Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 30, 2021 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo Michael Matomora alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Binilith Mahenge ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Kyengege Kata ya Kyengege.

Aidha amebainisha kwamba miradi yote imefikia hatua ya kupauliwa na tayari wasafirishaji wapo Dar es Salaam kuchukua mabati ambapo tunatarajia ndani ya siku mbili au tatu yatakuwa yamefika katika maeneo ya kazi, hivyo ni imani yetu kwamba mpaka tarehe tano tutakuwa tumemaliza kupaua kwa sababu tumesha nunua kila kitu, Alisema Matomora.

Mkurungezi huyo akabainisha kwamba katika miradi hiyo 47 ni ya ujenzi wa madarasa katika Shule za Sekondari 19 ambazo zitagharimu kiasi cha sh.Milioni 940

Aidha Mkurugenzi huyo akaeleza kwamba miradi 14 ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 14 katika shule shikizi saba (7) ambazo ni Ulongo, Magugu, Kagera, Itunda, Masunkune, Kisingu na Ibambasi ambazo zitagharimu kiasi cha Tsh. Milioni 280.

Amesema kwa ujumla Shule ambazo zinatekeleza miradi ya UVIKO 19 katika wilaya ya Iramba ni Lulumba, New Kiomboi, Kinambeu, Shelui, Kyengege, Kizaga, Kidaru, Mbelekese na Mtekente. Nyingine ni Mtoa, Tulya, Ntwike, Urughu, Ushora, Kinampanda, Mukulu, Mgongo, Kaselya na Kisiriri. alifafanua Matomora.

Akijibu baadhi ya changamoto zilizojitokeza kwenye utekelezaji wa miradi hiyo ikiwemo baadhi ya wakuu wa Shule kutotizimiza majukumu yao vizuri Mkuu wa Mkoa Dkt. Mahenge amesema Serikali haitamvumilia mtumishi yeyote wa Serikali atakaye sababisha uzembe katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Yeyote atakayefanya uzembe wa makusudi tutamchukulia hatua za kinidhamu ili iwe fundisho kwakwe na wengine wenye tabia kama hizo, lengo likiwa sio kumkomoa bali ni kwa ajili ya manufaa ya jamii husika. Alisema Dkt. Mahenge.

Hata hivo RC Mahenge amewapongeza viongozi wa wilaya ya Iramba kwa jitihada zao katika kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo ambapo mpaka sasa madarasa yote yamefikia hatua ya kupaliwa.

Aidha RC. Mahenge akawataka viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba pamoja na viongozi wa CCM kuendelea kusimamia kazi hizo na kuhakikisha kwamba inakamilika kabla au ndani ya Desemba 5, 2021.

Awali Suleiman Mwenda akimkaribisha Mkuu wa mkoa alisema wilaya inatekeleza miradi 47 ya ujenzi wa madarasa katika shule 19 ambapo jumla ya madarasa 18 yamefikia hatua kupauliwa katika shule saba (7)

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe. Suleiman Mwenda akiongea na walimu wa shule ya sekondari kinambeu.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.