• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, amefanya ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Posted on: July 10th, 2019

Wanachama wa CCM na wananchi wa wilaya ya Iramba wakimusikilza Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, katika ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Viongozi mbalimbali wakimuskiliza Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, katika ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, akiwa kwenye na wakinamama katika ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula, Mbunge wa jimbo la Iramba mashariki Mhe: Dkt Mwigulu Nchemba, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iramba Mhe: Samwel Ashery Joel na Diwani wa Kata ya Shelui wakiwa kwenye picha ya pamoja ya  kumkaribisha  Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, katika ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iramba Mhe: Samwel Ashery Joel akizungumza na wananchi kwenye ziara ya  Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mbuge Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe, akisalimia wananchi wa wilaya ya Iramba kwenye ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, 

wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mhe:Dkt Mwigulu Nchemba akizungumza na wananchi wa wilaya ya Iramba katika ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo,  wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mhe: Hassan Kilimba akizungumza na wananchi wa Iramba  katika ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo wilayani  Iramba mkoani Singida.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rodrick Mpogolo akizungumza na wananchi katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mhe: Rodrick Mpogolo, amefanya ziara ya kutembelea wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Mhe Mpogolo amekutana na wananchi wa Iramba akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mhe: Hassan Kilimba, mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mhe: Dkt Mwigulu Nchemba, Mhe Asyrose Mattembe mbunge viti maalum (CCM) viongozi mbalimbali wa mkoa wa singida na viongozi wa wilaya ya Iramba.

Mhe: Mpogolo akizungumza na wananchi amesema “Nawashukuru sana kwa Mapokezi makubwa, nimefurahi sana, nawashukuru sana kwa moyo wenu wa dhati Mwenyekiti wa CCM wilaya, Mkuu wa wilaya ya Iramba, Mwenyekiti wa Halmashauri na madiwani wote, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba na watendaji nawashukuru kwa kazi mnazozifanya kwa ajili ya kuwaletea wananchi wa Iramba maendeleo alisema Mhe: Mpogolo

Aliongeza kusema “Mhe: Rais Dkt, John Pombe Joseph Magufuli  anawasalimu sana wananchi wa Iramba, Rais anawapenda wananchi wa Iramba pamoja na watanzainia wanyonge kama sisi, serikali yenu ipo kwa kutatua changamoto za wananchi alisema Mhe: Mpogolo

Tanzania inasonga mbele kwa kasi kubwa sana, Watanzania tunabahati kwa sababu Mhe: Rais anawapenda watanzania naomba tumuunge mkono kwa dhati kabisa kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa nchi yetu, anafanya mambo makubwa sana Watanzania tunajivunia sana na Rais wetu, aliongeza kusema Mhe: Mpogolo

Amewambia Watendaji waendelee kuchapa kazi na wahakikishe miradi yote inayotekelezwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za kijamii ziwe na viwango vinavyoridhisha, “miradi ya kijamii itekelezwe katika kiwango bora, inasaidia kupunguza gharama zisizokuwa za lazima na kuwawezesha wananchi kupata kwa wakati mahitaji muhimu ya kijamii.

Mhe: Mpogolo amewaasa viongozi mbalimbali na wananchi wa Iramba kuheshimiana na kuwa na mshikamano kwa ajili ya kujenga nchi yetu kwa pamoja, “Shariti la kwanza la katiba ya CCM lazima kuheshimu watu, Viongozi wa CCM tunapaswa kuwaheshimu waliokuchagua, lazima kwenye chama tuwe na heshima, tuheshimu wananchi wetu. Tunahitaji CCM yenye mshikamano ili tuwahudumie wananchi wetu na kuwaletea maendeleo. Binadamu wote ni sawa, kila mmoja anastahili heshima na kutambuliwa utu wake. lazima mshirikiane kwa pamoja ili tuweze kuleta maendeleo ya kweli. Tunaenda kufanya uchanguzi wa serikali za mitaa, na Kuboresha daftari la tume ya taifa la wapiga kura, tushirikiane Kutambua vijana wote ambao wanasifa za mpiga kura, wote waandikishwe alisistiza Mhe: Mpogolo

Mbunge wa Iramba Magharibi Mhe: Dkt Mwigulu Nchemba ametoa pongezi za dhati kwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya Afya vya Ndago na Kinampanda, kuleta umeme, ujenzi wa madaraja, maji, ujenzi wa mabweni na miradi mingi katika wilaya ya Iramba. “Namshukuru sana Rais Magufuli kwa Ujenzi wa vituo vya afya vya Ndago na Kinampanda, sisi huku hatuiti vituo vya afya bali tunaviita hospitali, Ujenzi wa madaraja, kutuletea umeme, ujenzi wa mabweni kwa ajili wa wanafunzi wetu, uchimbaji na usambazaji wa Maji na miradi mingi alisema Dkt. Nchemba.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.