• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

SHILINGI MILIONI 99 ZIMETUMIKA KUKAMILISHA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MASAGI KILICHOPO KATA YA MTOA, TARAFA YA SHELUI WILAYA YA IRAMBA MKOANI SINGIDA.

Posted on: May 8th, 2023

SHILINGI MILIONI 99 ZIMETUMIKA KUKAMILISHA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MASAGI KILICHOPO KATA YA MTOA, TARAFA YA SHELUI WILAYA YA IRAMBA MKOANI SINGIDA.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleimani Yusuph Mwenda;  Amezindua rasmi Zahanati ya Kijiji cha Masagi Kata ya Mtoa Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Zahanati ambayo inakusudiwa kuhudumia wananchi wapatao 3,117 katika Kijiji hicho Cha Masagi.

 Aidha DC Mwenda,Akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi, kwa lengo la kushuhudia uzinduzi wa Zahanati hiyo amewataka wananchi hao kuhudhuria kikamilifu na Kupata matibabu katika Zahanati hiyo, kwani kwa sasa changamoto ya kufuata matibabu kwa mwendo mrefu umeisha.

Mwenda Amesema kuzinduliwa kwa Zahanati hiyo kutaondoa  kabisa vifo vya akina Mama na watoto  ambao walikuwa wanayapata  wakati wanafuata Matibabu Shelui au Mtoa  na halikadhalika katika Hospitali ya Wilaya.

Mkuu huyo wa Wilaya, Amesema kwa sasa vifo vya akina mama vitapungua kwa asilimia kubwa  kutokana na kukamilika kwa Zahanati nyingi katika vijiji Wilayani Iramba, lakini pia pindi vituo vya Afya vya Mtoa, na Shelui vitakapokamilika vitafanya vifo vya mama na mtoto kuwa ni historia katika nchi.

Aidha Mwenda amebainisha kuwa Mpaka sasa,Tayari Tsh. Milioni 280 zimeletwa kumalizia Kituo cha Afya Mtoa, Huku jumla ya Tsh.Milioni 120 zimeingia tayari kwa ajili ya Kukamilisha Kituo Cha Afya Shelui, na kuongeza kuwa tayari shilingi Milioni 200 zimeletwa Kukamilisha ujenzi wa  Zahanati ya Kinambeu  Ili kuhudumia wananchi wa eneo hilo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba Dkt. Hussein Sepoko amesema  Zahanati ya Masagi  imekamilika na tayari imepewa  Vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi  Milioni 24 huku wahudumu wa Afya wawili tayari wamefika  kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

Aidha wananchi wa Kijiji hicho wameishukuru serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali kuhusiana na Afya zao na sasa wamepona kilio chao cha muda mrefu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.