• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Katiba na Sheria, Frofesa Palamagamba Kabudi amewataka vijana wote Nchini kuona fahari ya kuzaliwa Tanzania.

Posted on: August 4th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Waziri wa Katiba na Sheria, Frofesa Palamagamba Kabudi amewataka vijana wote Nchini kuona fahari ya kuzaliwa Tanzania.

Kabudi ametoa wito huo leo Jumanne Agosti 4, 2021 wakati akiongea na watumishi wa kada tofauti wilayani Iramba Mkoa wa Singida katika ukumbi Mkubwa wa Halmashuri hiyo alipofanya ziara yake mjini hapo.

Akiongea na watumishi hao, Waziri Kabudi amesema kuwa Tanzania ni moja kati ya Nchi chache Barani Afrika na Duniani kwa ujumla iliyofanikiwa kujenga utaifa.

“Watumishi wenzangu fahamuni kuwa Tanzania na hasa vijana muone fahari mmezaliwa watanzania na leo hamjazaliwa na makabila yenu, muwe na fahari kwani Tanzania ni Taifa ambalo limejiwekea misingi inayojali watu wote” amesema Prof. Kabudi nakuongeza kuwa

“Sisi ni Taifa, la uchumi wa kati, lililopita katika misukosuko na dhuruba lakini limebaki kuwa imara na linasonga mbele chini ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan.”

Akieleza lengo la ziara yake Wilayani hapo kuwa ni kuona utendaji wa haki, demokrasia, utawala bora na utawalaya wa sheria kwa namna ambavyo vilieelekezwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) vinatekelezwa kwa sababu ndio chama kinachoisimamia Serikali.

Aidha amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya hiyo, Suleiman Mwenda kuwa yeye ni mahiri na kuwa ataweza kuingoza Wilaya hiyo kupitia Ilani ya Chama.

Awali akiwasilisha hali ya utendaji wa haki, utawala bora na utawala wa sheria katika wilaya hiyo mbele ya Waziri huyo, Mkuu huyo wa Wilaya, Suleiman Mwenda amesema kuwa Wilaya imeendelea kutekeleza shughuli zake kwa kufuata misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha kunakuwepo uwazi, uwajibikaji, ushirikishwaji, utawala wa sheria na majadiliano.

Mwenda amefafanua kuwa Wilaya imefanikiwa kuhakikisha inawajibika ili wananchi wapate huduma za msingi kwa wakati na kiwango kinachotakiwa.

Aidha amebainisha kuwa serikali ya wilaya imefanikwa kuendesha shughuli zake kwa uwazi na kufanikiwa kuwapa fursa wananchi kupata taarifa zote muhimi zinazohusu mipango na makusanyo ya fedha na matumizi yake yanabandikwa katika mbao za matangazo, hivyo kuwapa fursa wananchi kujuwa nini kinaendelea katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya hiyo, Ibrahim Mjanaheri amemshukuru Waziri huyo kwa namna walivyorekebisha sheria ya madini na kuhakikisha rasilimali za Nchi zinabaki kuwanufaisha watanzania.

Pia amemuomba kutoa kipaumbele cha ujezi wa Mahakama ya Wilaya ya kisasa ijengwe Wilayani hapo kwa sababu itasaidia kutoa taswira nzuri ya wilaya.

Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi anayeshughulikia Wilaya ya Iramba na Mkalama, Christopher Makwaya ameseama kuwa Mahakama imekuwa na spidi ya kuendesha mashauri kwa njia ya kidigitali.

Makwaya amesema kuwa hali hiyo inasaidia kupata nakala ya hukumu punde tu baada ya shauri la mtuhumiwa kukamilika na kufanikiwa kusogeza huduma kwa wananchi.

MWISHO

Waziri wa Katiba na Sheria, Frofesa Palamagamba Kabudi katikati akiwa katika picha na ya pamoja na baadhi ya viongozi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya iramba, Suleiman Mwenda na Kulia ni Katibu wa Chama cha Mapinduzi  (CCM) Ibrahim Mjanaheri. Picha na Sarapion Kakiziba

Viongozi mbalimbali wakifuatilia nasaha za Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi ukumbi Mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Sarapion Kakiziba

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.