• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia Suluhu Hassan amefanya ziara ya kukagua na kutembelea miradi mbalimbali wilayani Iramba Mkoani Singida.

Posted on: February 20th, 2019

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia Suluhu Hassan amefanya ziara ya kukagua na kutembelea miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya cha Kinampanda, Ukarabati wa chuo cha Ualimu Kinampanda, Kiwanda cha kukamua Mafuta ya alizeti cha YAZA tarafa ya Ndago na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Akizungumza na wananchi wa Iramba, makamu wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia Suluhu Hassan amewapongeza wananchi wa Iramba katika kushiriki kwenye shughuli za maendeleo. “Nawapongeza sana wananchi wa Iramba kwa Mapokezi makubwa, mmejitokeza kwa wingi na mmekuwa mstari wa mbele kushirikiana katika shughuli za maendeleo kwa nguvu zenu zote. Dumisheni ushirikiano, Amani na utulivu ndani ya maeneo yenu Alisema Mhe: mama Samia.

Makamu wa Rais, alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa mkoa wa Singida kwa kile alichodai kwamba toka ameanza ziara yake hadi anamaliza, ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ambayo ina thamani inayofanana na fedha zilizotumika.

Aidha makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia Suluhu Hassani ameagiza leseni 40 zilizo futwa na Wizara ya Madini Mkoa wa Singida wapewe wazawa wachimbe ili waweze kunufaika na kuleta Maendeleo katika Mkoa wa Singida.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo baada ya Waziri wa Madini, Mhe: Dotto Biseko, kusema wamefuta leseni hizo baada ya wahusika kushindwa au kuchelewa kuanza kuchimba madini hayo kwa wakati.

Mama Samia ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wakazi wa wilaya ya Iramba muda mfupi baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa kituo cha afya cha Kinampanda na maboresho na ukarabati wa chuo cha Ualimu Kinampanda pamoja na kiwanda kikubwa cha Yaza cha kukamua mafuta ya alizeti ambacho kinamilikiwa na Yusuph Nalompa mkazi wa Ndago,

Alisema serikali ya awamu ya tano inapenda kuona wazawa wakinufaika zaidi na rasilimali mbalimbali ikiwemo madini. “Kwa maoni yangu napendekeza maeneo ambayo leseni zake zimefutwa, wapewe vijana wachimbe na Mapato watakayopata, wahakikishe wanalipa kodi stahiki na kwa wakati ili serikali iweze kugharamia miradi ya maendeleo ya wananchi” alisisitiza Mhe: Mama Samia.

Katika hatua nyingine, Mhe: Mama Samia amewataka wakazi Iramba Mkoa wa Singida, wenye sifa za kupiga kura, wajitokeze kwa wingi kuchangua viongozi wa serikali za mitaa watakaoendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano. “Uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu, utumike kuchangua viongozi wenye uwezo wa kufanya kazi na kwenda haraka na sera za serikali kusimamia miradi yetu na kutuletea maendeleo. Wawe ni watu madhubuti ndani ya mioyo yao, wawe na uzalendo wa kweli. Tukichangua viongozi bora, tutakuwa tumeweka msingi mzuri na imara kwa ajili ya uchanguzi mkuu utakaofanyika mwakani”alisisitiza Mhe: Mama Samia.

Aliongeza kusema, Tuhakikishe kituo cha afya cha Kinampanda kinamalizika ili serikali ilete Watumishi, vifaa tiba pamoja na dawa ili wananchi waweze kupata huduma. Hatuna changamoto ya Dawa, vifaa tiba wala Watumishi. itategemea na sipidi yenu ya kumaliza ujenzi wa kituo cha afya cha Kinampanda alisisitiza Mhe: mama Samia

Kuhusu gonjwa la UKIMWI, Makamu wa Rais, alisema mkoa wa Singida hauko vizuri katika maambukizi ya VVU, kwa madai kuwa maambukizi kwa sasa ni asilimia 3.6 ambapo miaka ya nyuma ilikuwa asilimia 3.1. “Taarifa nilizonazo ni kwamba wanaume wa mkoa huu, sasa wanakimbilia zaidi wasichana wenye umri mdogo kwa imani kwamba hawajaambukizwa UKIMWI. Hawawakimbilii wanawake wenye umri mkubwa, wakiamini kuwa wengi wao hawapo salama, alisema Mhe: Mama Samia “Kwa ujumla nitoe onyo kwamba UKIMWI bado hauna chanjo wala tiba, kila mtu achukue tahadhara na gonjwa hili baya”.

Serikali imekuja na mpango wa sheria ya Bima ya afya ambapo kila Mtanzania anatakiwa kuwa na bima ya afya. Kila mtanzania anatakiwa kuwa na Bima ya afya na itatolewa kwa gharama nafuu, hii ni kwasababu kila mtanzania aweze kutibiwa kwa gharama nafuu sana na malazi yanapokuja hayakupi taarifa lakini ukiwa na bima ya afya utapata huduma kwa gharama nafuu alisisitza Mhe: mama Samia.

Akizungumza juu ya kumaliza changamoto ya maji wilayani Iramba, Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia Suluhu Hassan amesama Mradi wa uchimbaji wa visima 3 vya maji kata ya Mgongo, tunategemea baada ya uchimbaji wa visima hivi kukamilika vitakuwa na uwezo wa kutoa takribani lita milioni 2.1 kwa siku. Nia ya serikali ni kuhakikisha watanzania wote wanapata maji safi na salama na ifika mwaka 2020 vijiji vyote Tanzania vitapata maji safi na salama kwa asilimia 85 na maeneo ya mijini yatapata maji kwa asilimia 100 alisema Mhe: Mama Samia.

Aliongeza kusema “kuna mradi mwingine wa maji unatokea ziwa victoria kuleta maji Tabora, Igunga na Tarafa ya Shelui ambao utagawa maji katika vijiji vyote vya Shelui ili kuhakikisha watanzania wanapata maji safi na salama.

Akizungumza katika mkutano huo, Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe: Mama Samia alisema umeme ufungwe Kijiji kwa Kijiji, Kitongoji kwa Kitongoji, Nyumba kwa Nyumba bila kuruka nyumba yoyote, Wananchi wote wafungiwe umeme kwa elfu 20000 na kila kijiji kipate umeme  wilayani Iramba. alisisitiza Mhe. Mama Samia.

Ameagiza Halmashauri ya wilaya ya Iramba kuhakikisha inapeleka fedha zilizotengwa kwa ajili ya Vijana na wanawake. “Uwezeshaji wa vijana na wanawake lazima ufanyike. Hizi fedha zinatengwa kwa ajili ya kuwezesha vijana na wanawake, hii ni haki yenu, Vijana lazima mdai hizi fedha kutoka Halmashauri kwa sababu ni haki yenu.

Vile Vile amewashauri kuacha kukata miti ili kuwa na mazingira bora. Amewaasa wananchi katika wilaya ya Iramba kutunza mazingira, Kupata mvua ya kutosha pia kuifadhi mfumo wa maji kwa maendeleo ya jamii “Naomba mujitahidi kupanda miti ili turudishe hali nzuri ya ya hali ya hewa. Mtunze mistu kwani ndo uhai wetu, tunza mazingira ili mazingira yatutunze” Alisisitiza Mhe: Mama Samia

Amemwagiza Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula kuhakikisha anasimamia migogoro ya ardhi, amewataka Viongozi ngazi ya wilaya, tarafa, kata na kijiji kushirikiana kutatua migogoro ya wananchi. “hatutaki kusikia wananchi wamepigana, wamejinyonga kwasababu ya migogoro ya ardhi alisisitiza Mhe:Mama Samia

Wakati huo huo, Waziri wa Madini, Mhe: Dotto Biteko, alitumia mkutano huo kutoa onyo kwa watu ambao wanadhani sekta ya madini bado ni mahali pa kuchezea, watakuwa wanakosea sana. “Sasa hivi tumejipanga vizuri kuhakikisha Madini yananufaisha Watanzania na si vinginevyo. Tumechezewa sana, watu ambao si wazawa, wamenufaika mno na madini yetu. Matarajio yetu sasa, ni Watanzania kunufaika. Tuna uhakika huo, kutokana na serikali ya awamu ya tano, imekutunga sheria mpya ambazo hazitoi nafasi kunufaisha watu kutoka nje ya nchi” alisema Mhe: Biteko

Mbunge wa jimbo la Iramba, Mhe: Dkt. Mwigulu Nchemba ameishukuru serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe: Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwa kutoa shillingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya Ndago na Kinampanda na Gari la kubebea wagonjwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.