• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa latekelezwa Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Posted on: November 13th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaagiza wananchi kwenda kuchukuwa mbegu za pamba na kulima kwa tija.

Luhahula ameyasema hayo leo Ijumatano Novemba 13, 2019 wakati akiwa katika ziara ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali kitongoji  cha Lutamla kijiji cha Msai kata ya Mtoa Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida Tanzania.

Ziara hiyo ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Kassim  Majaliwa alipo fanya ziara Wilayani hapo Oktoba 6, 2019 ambapo aliagiza kutumia siku  4 kwenda vijijini kusikiliza  kero za wananchi  na kuwaelimisha mambo mbalimbali yanayopatikana katika  kila sekta na   namna ambavyo watakavyoweza kunufaika kupitia sekta hizo.

 

Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka wananchi kupanda  kitaalamu ambapo hekari moja iwe na mashina 22,000 kwa mbegu ya pamba huku mbegu ya mahindi ifike mashina 18,000.

Luhahula amepongeza uuzaji wa pamba kuwa mzuri Wilayani hapo hali ambayo iliwafanya watu kutoka na Wilaya ya Meatu na Wilya ya Igunga kuja kuuza pamba, huku akiwataka wananchi kuwa na imani  kuwa watalipwa fedha zao zilizobakia kwani  Mnunuzi wa pamba alikuwa anadaiwa 700 milioni na sasa  amebakiza   60 milioni ambazo Ijuma hii anakuja kuzimalizia.

 Amewataka wananchi wa Mtoa kuacha vitendo vya kihalifu huku akiwatahadharisha mabalozi wote wanaoshindwa kuwabaini wanaotenda uhalifu katika maeneo hayo.

Halikadhalika amewataka wazazi kuwalinda watoto kutokana na vifo vinavyotokana na uzembe na kuwaonya  wavulana na wanaume kuacha kuwachezea watoto wa shule na kuwapa mimba kwani hatua kali zitachukuliwa dhizi ya yule atakayempa mimba mwanafunzi.

“Mtoto wa shule ni wakwako kwa kuwa umemzaa lakini akiwa shuleni ni wakwangu mimi serikali, acheni kuelewana kupeana ng’ombe kwa mapatano ya waliowatia mimba wanafuzi,” amesisitiza Luhahula

Kwa upande wa afya Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka wananchi kujiunga na  CHF iliyoboreshwa inayowawezesha kutibiwa wilaya yoyote Mkoani Singida kwa garama ya 30,000 tu kwa mwaka.

Akiwa ziarani hapo Mkuu wa Wilaya hiyo ameambatana na Maafisa mbalimbali waliotumia nafasi hiyo kuwaelimisha wananchi mambo mbalimbali.

Akiongea katika ziara hiyo  Afisa Kilimo, Mwampashe Zawadi amewataka wananchi kufanya maandalizi ya kilimo kwa kusafisha mashamba, kuchoma masalia ya msimu uliopita na kuandaa pembe jeo.

Naye Afisa Afya wa Halmashauri hiyo, Salome Mwaipopo amewaagiza wananchi kuwa na vyoo vinavyoweza kuhimili masika, kiangazi, kuweka milango na paa katika vyoo hivyo.

Hatuwa hiyo itasababisha kutunza mazingira na kuepuka magonjwa ya mlipuko  kama vile kipindupindu, homa za matumbo na mengineyo.

Akisisitiza suala la afya ya uzazi kwa wakinamama hao, Mwaipopo amewataka wakinamama wanaopata ujauzito kufika mapema kwenye vituo vinavyotoa huduma za afya huku akiwataka wakinababa kuwasindikiza wakinama.

Kwa upande wake Afisa wa kuzuwia na kupambana na rushwa wilayani hapo, Benjamini Masyaga amewaelimisha wananchi rushwa ndogo na kubwa huku akiwataka kujiepusha nazo na kutoa taarifa  Ofisi ya Mkuu wa Wilaya jambo lolote  la rushwa.

“ Rushwa ni fedha au kitu cha thamani anachopewa  mtu mwenye madaraka ya jambo fulani ili mtoaji apate upendeleo” ameelimisha

Akibainisha madhara yatokanayo na rushwa katika jamii, Masyaga emeongeza kuwa rushwa inapokomaa hufanya maendeleo kutokuwepo na utu wa mtu kununuliwa.

Aidha amewataka wananchi kutambuwa jukumu lao la kusimamia fedha yoyote ya maendeleo itakayokuwa imeletwa kijijini hapo huku akiwata wadai kusomewa mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu na kutoa taarifa pindi viongozi wasiposoma mapato na matumizi.

Mkuu wa Wilaya hiyo amefanya ziara kijiji cha Msai na Masagi Wilayani humo.

Msai ni eneo maarufu kwa ulimaji wa pamba ambapo 2011 sherehe za pamba kitaifa zilifanyika hapo.                                                                                                                                                                                                                              

Afisa Kilimo Wilayani Iramba, Mwampashe Zawadi akifafanua mambo mbalimbali yanayohusu kilimo kwa wananchi wa Msai kata ya Mtoa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga                                                                      

Afisa wa kuzuwia na kupambana na rushwa  Wilayani Iramba, Benjamini Masyaga  akielimisha  mambo mbalimbali yanayohusu rushwa kwa wananchi wa Msai kata ya Mtoa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga              

Afisa Afya Wilayani Iramba, Salome Mwaipopo  akielimisha  mambo mbalimbali yanayohusu afya ya uzazi, mazingira na CHF iliyoboreshwa kwa wananchi wa Msai kata ya Mtoa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga       

Wananchi wa Msai wakifuatilia kwa makini wataalamu mbalimbali walioongozana na Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula katika ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wilayani hapo. Picha na Hemedi Munga                            

Wananchi wa Msai wakifuatilia kwa makini wataalamu mbalimbali walioongozana na Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula katika ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wilayani hapo. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.