• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ahadi ya Rais John Pombe Magufuli kwa Maafisa Tarafa yatimizwa Wilayani Iramba.

Posted on: March 20th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amekabidhi pikipiki nne kwa Maafisa Tarafa wa Tarafa ya Kinampanda, Kisiriri, Ndago na Shelui.

Makabidhiano hayo ameyafanya leo Ijumaa Machi 20, 2020 mbele ya jengo la Mkuu wa  Wilaya ya Iramba mjini hapa.

Luhahula amewaomba Maafisa Tarafa hao kuzitunza pikipiki hizo na kuzitumia kuleta maendeleo na kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

“ Na sasa ninaamini mtafanya majukumu yenu kwa kasi zaidi, ninaomba mzitunze kwa kuwa ni mali ya Serikali japokuwa mmekabidhiwa nyinyi,” amesema Luhahula na kuongeza

 

“ Tuko katika kampeni ya kuzuia na kuelimisha wananchi kuhusu ugonjwa wa korona, tumieni pikipiki hizi kuzunguka katika maeneo yenu kuhakikisha wananchi wameweka maji ya kunawa na sababuni pamoja na dawa za kupaka.”

Amewaagiza Maafisa Tarafa hao kuhakikisha kuwa ofisi zote za umma  na binafsi zinakuwa na vyombo vyenye maji na sabuni pamoja na kufuata maelekezo ya wataalam wa Afya.

“ Hakikisheni kuwa vifaa vya kunawia vimewekwa mpaka kwenye ofisi za watendaji wa vijiji ili kuilinda Iramba pamoja na Taifa letu,” amesema Luhahula

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amesema kuwa Serikali inaendelea kutoa elimu mbalimbali namna ya kujikinga na visuri vya korona kwa kufuata maelekezo ambayo yanatolewa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.

“Tunaendelea kutoa elimu ya kuzingatia usafi wa kila unapotoka kwenye tukio moja kwenda kwenye tukio lingine kunawa maji yanayo tiririka kwa sabuni na kuhakikisha wananchi wanaepuka mikusanyiko mikubwa kwenye maeneo mbalimbali,” amesama Mwageni

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Pius Songoma amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi ambayo aliwaahidi Maafisa Tarafa Nchi nzima kuwapatia vitendea kazi.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya pikipiki hizi ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ameitekeleza,” amesema Songoma

Akiongea katika makabidhiano hayo kwa niaba ya Maafisa Tarafa wa Wilaya ya Iramba, Mwenyekiti wa Maafisa Tarafa hao, Nicholas Mokoye amesema kuwa watatumia pikipiki hizo kuhamasisha na kufuatilia wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na virusi vya korona.

“ Sisi kuwa na pikipiki hizi ni faraja kwetu kwa kuwa tutaweza kufika maeneo yote na kufanya  kazi zetu kuwa nyepesi na rahisi sana,” amesema Makoye

Amesema kuwa watatumia pikipiki hizo  kutekeleza majukumu na kusimamia miradi yote inayotekelezwa  katika Tarafa zao.

MWISHO

Afisa Tarafa wa Tarafa ya Shelui, Nicholas Makoye  akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi yake aliyowaahidi Maafisa Tarafa Nchi nzima wakati alipoongea nao Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na Hemedi Munga

Fundi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Ndugu Matoto akizikagua pikipiki kabla ya kuzigawa kwa maafisa Tarafa wa Tarafa ya Kinampanda, Kisiriri, Ndago na Shelui. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.