• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Baraza la Madiwani Wilayani Iramba lamfuta kazi Mtumishi wa Idara ya Afya kwa tuhuma za utoro kazini.

Posted on: June 3rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Baraza la Madiwani Wilayani Iramba, limemfukuza kazi Mtumishi wa Idara ya Afya, Muuguzi Daraja la tatu Rashidi Abed kwa tuhuma za kutokua kazini kwa zaidi ya siku tano.

Maamuzi hayo yametolewa leo Juni 2, 2020 na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo katika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri Mjini Hapa.

Akitanganza maamuzi ya kikao cha kamati ya nidhamu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela amesama baada ya Baraza kujigeuza kuwa Mamlaka ya kinidhamu katika moja ya ajenda zake imemfuta kazi mtumishi huyo.

“Mtumishi Rashid Abed Muuguzi Daraja latatu ambae amepatikana na tuhuma ya kutokua kazini zaidi ya siku 5 na katika mahojiano na timu iliyomchunguza amedai kuwa hataki kufanya kazi Iramba,” amesema Tyosela na kuongeza

“Na sisi kwa mamlaka tulionayo tumemfuta kazi, hafanyi kazi Iramba na akatafute sehemu ambayo anahitaji yeye.”

Pia, kikao hicho kimewathibitisha kazi Wakuu wa Idara wawili, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya hiyo, Dkt. Hussein Sepoko na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo, Jane N’gondi.

Halikadhalika, Kikao hicho kimepitisha jina la Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi ambalo limependekezwa.

“Tumepitisha jina ambalo limependekezwa la Mkurugunzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi, Ndugu Shiwariel Marunda.” Amesisitiza Mwenyekiti huyo na kutolea ufafanuzi

“Kikao kimewathibitisha kazini Watumishi saba wa kada ya utendaji wakata.”

Akiongea kwa njia ya Simu na Muandishi wetu, Mkurugenzi Mteule wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi, Shiwariel Marunda amewashukuru Wajumbe wote kwa kukubali kumteua kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi.

“Ninawashukuru Wajumbe wote kwa kuafiki mimi kupewa jukumu hilo ninaahidi nitatumika kwa kadri ya uwezo wangu kuitumikia Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Taifa letu la Tanzania,” ameshukuru Marunda na kuongeza

“Kwa kweli tumepewa jukumu la kuhakikisha kwamba Wanairamba wanapata maendeleo na hasa tutajikita kutatua changamoto zao ambazo wamepewa Mji wanamatumaini kuwa zitaondoka.”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amewaomba Madiwani hao kuendelea kushirikiana kuhakikisha wanamaliza awamu hii ya uongozi salama.

“Baraza lako tukufu sina mashaka nalo kwa namna ambavyo tumeshirikiana katika miaka hii, hivyo niombe tuendelee kushirikiana ili tumalize vizuri.” amesema Mwageni

Naye Diwani wa Kata ya Shelui na Mwenyekiti wa Huduma za Jamii wa Halmashauri hiyo, Omary Kinota amewaomba Madiwani kuhakikisha wanawaeleza Wananchi waliopo katika maeneo yao kuhakikisha wanahifadhi chakula kwa kuwa baadhi ya maeneo hawakubahatika kupata mavuno mazuri kutokana na changamoto za mvua za mwaka huu.

Mkutano wa Baraza la Madiwani umefanyika leo na kuchakata dondoo mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri na miradi ya maendeleo katika kata zote inakwenda vizuri.

MWISHO

  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akijibu maswali ya hapo kwa hapo toka kwa Madiwani Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakifuatilia hoja mbalimbali Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.