• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Baraza la Madiwani Wilayani Iramba lamfuta kazi Mtumishi wa Idara ya Afya kwa tuhuma za utoro kazini.

Posted on: June 3rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Baraza la Madiwani Wilayani Iramba, limemfukuza kazi Mtumishi wa Idara ya Afya, Muuguzi Daraja la tatu Rashidi Abed kwa tuhuma za kutokua kazini kwa zaidi ya siku tano.

Maamuzi hayo yametolewa leo Juni 2, 2020 na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo katika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri Mjini Hapa.

Akitanganza maamuzi ya kikao cha kamati ya nidhamu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela amesama baada ya Baraza kujigeuza kuwa Mamlaka ya kinidhamu katika moja ya ajenda zake imemfuta kazi mtumishi huyo.

“Mtumishi Rashid Abed Muuguzi Daraja latatu ambae amepatikana na tuhuma ya kutokua kazini zaidi ya siku 5 na katika mahojiano na timu iliyomchunguza amedai kuwa hataki kufanya kazi Iramba,” amesema Tyosela na kuongeza

“Na sisi kwa mamlaka tulionayo tumemfuta kazi, hafanyi kazi Iramba na akatafute sehemu ambayo anahitaji yeye.”

Pia, kikao hicho kimewathibitisha kazi Wakuu wa Idara wawili, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya hiyo, Dkt. Hussein Sepoko na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo, Jane N’gondi.

Halikadhalika, Kikao hicho kimepitisha jina la Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi ambalo limependekezwa.

“Tumepitisha jina ambalo limependekezwa la Mkurugunzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi, Ndugu Shiwariel Marunda.” Amesisitiza Mwenyekiti huyo na kutolea ufafanuzi

“Kikao kimewathibitisha kazini Watumishi saba wa kada ya utendaji wakata.”

Akiongea kwa njia ya Simu na Muandishi wetu, Mkurugenzi Mteule wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi, Shiwariel Marunda amewashukuru Wajumbe wote kwa kukubali kumteua kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi.

“Ninawashukuru Wajumbe wote kwa kuafiki mimi kupewa jukumu hilo ninaahidi nitatumika kwa kadri ya uwezo wangu kuitumikia Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Taifa letu la Tanzania,” ameshukuru Marunda na kuongeza

“Kwa kweli tumepewa jukumu la kuhakikisha kwamba Wanairamba wanapata maendeleo na hasa tutajikita kutatua changamoto zao ambazo wamepewa Mji wanamatumaini kuwa zitaondoka.”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amewaomba Madiwani hao kuendelea kushirikiana kuhakikisha wanamaliza awamu hii ya uongozi salama.

“Baraza lako tukufu sina mashaka nalo kwa namna ambavyo tumeshirikiana katika miaka hii, hivyo niombe tuendelee kushirikiana ili tumalize vizuri.” amesema Mwageni

Naye Diwani wa Kata ya Shelui na Mwenyekiti wa Huduma za Jamii wa Halmashauri hiyo, Omary Kinota amewaomba Madiwani kuhakikisha wanawaeleza Wananchi waliopo katika maeneo yao kuhakikisha wanahifadhi chakula kwa kuwa baadhi ya maeneo hawakubahatika kupata mavuno mazuri kutokana na changamoto za mvua za mwaka huu.

Mkutano wa Baraza la Madiwani umefanyika leo na kuchakata dondoo mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri na miradi ya maendeleo katika kata zote inakwenda vizuri.

MWISHO

  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akijibu maswali ya hapo kwa hapo toka kwa Madiwani Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakifuatilia hoja mbalimbali Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.