• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Baraza la Madiwani wilayani Iramba Mkoa wa Singida limepitisha takribani Tsh 41.163 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na mipango ya maendeleo kutoka kwenye vyanzo vya Halmashauri, Ruzuku ya Serikali, Wahisani na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Posted on: February 23rd, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Baraza la Madiwani wilayani Iramba Mkoa wa Singida limepitisha takribani Tsh 41.163 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na mipango ya maendeleo kutoka kwenye vyanzo vya Halmashauri, Ruzuku ya Serikali, Wahisani na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Baraza la Madiwani limepitisha bajeti hiyo leo Februari 22, 2022 katika kikao cha mapendekezo ya makasio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano mjini hapa.

Akiongea katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Innocent Msengi aliwataka Madiwani kwa kushirikiana na Wakuu wa Idara na Vitengo kutambua kuwa bajeti hiyo itafikiwa ikiwa watadumisha ushirikiano wa kusimamia ukusanyaji wa mapato.

“ Niwaombe sana Madiwani na Wakuu wa Idara kutambua kuwa mzigo huu wa kukusanya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti hii ni wetu, hivyo tujitoe kwa dhati ili Iramba iendelee kuhudumia wananchi wake kwa weledi wa hali ya juu.” Alisema

Bajeti hii imekuwa ya mfano ukilinganisha na bajeti iliyopita ambapo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ilikisia kukusanya takribani Tsh 34.174 bilioni wakati mwaka wa fedha 2022/2023 ikikisia kukusanya takribani Tsh 41.163 bilioni.

Akitoa salamu za Serikali mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda aliwakumbusha Madiwani pamoja na Wataalamu wote kuhakikisha maadalizi ya Sensa ya Watu na makazi ya mwaka 2022 yanafanyika kwa weledi mkubwa ili kufanikisha azma ya serikali ya kutoa huduma kwa wananchi kikamilifu.

Mwenda alifafanua kuwa Sensa ya Watu na Makazi itasaidia kupata takwimu sahihi kwa ajili ya kuiwezesha serikali kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi wake.

Aidha, alisema kuwa zoezi hili litakuwa na faida kubwa kwa nchi na raia wake kutambua idadi ya watu na makazi yao, hivyo ni rahisi serikali kupanga bajeti ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kulingana na mahitaji ya jamii katika kila eneo.

Halikadhalika, aliwataka Madiwani kwa kushirikiana na Wataalamu kutekeleza agizo la serikali la upangaji wa postikodi kwa ajili ya anuani za makazi kwa sababu kutarahisisha mawasiliano na utoaji wa huduma za msingi kwa wanawake.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora aliwashukuru wadau wote kwa namna walivyoshirikiana kufanikisha rasimu ya bajati ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Aidha, amewaomba wajumbe hao kufahamu kuwa watatumia fedha kufuatia mipango iliyopo katika bajeti ambayo wameipitisha.

“Niwashukuru wadau wote kwa kushiriki kuandaa rasimu ya bajeti na kutoa wito kuwa mchakato huu ni endelevu bado tunaendelea kupokea maelekezo ya serikali kwa namna ambavyo itaona inafaa.” Alisisitiza  

Aidha, alibanisha kuwa katika suala la kukusanya fedha haitarajiwi mkusanyaji fedha kupendwa na kila mtu, hivyo endapo Madiwani watasikia malalamiko basi wayapokea kwa mtazamo chanya kwa lengo la kukusanya fedha tu, kwa sababu fedha pekee ndio inapendwa na kila mtu.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mtekente wilayani humo, Nowel Shole alichangia katika bajeti hiyo kuongeza umakini na usimamizi katika mazao ya misitu kukusanya mapato ili kuhakisha bajeti hii inatekelezeka.

Iramba imekuwa na misitu ya hifadhi mingi ambapo hapo awali walikuwa hawakusanyi ushuru, hivyo katika bajeti hii waingizaji wa mifugo na watakaokamatwa katika uchomaji na uuzaji wa mkaa watatozwa ushuru.

Naye Albert Makala Diwani wa kata ya Mtwike wilayani humo alisema kuwa katika bajeti hii kunaongezeko la takribani asilimia 26 ukilinganisha na bajeti ya mwaka jana, hivyo aliiomba Halmashauri ijikite kutekeleza miradi ya maendeleo na kuhakikisha miondombinu ya barabara inapewa kipaombele ili kurahisisha mawasiliano ambayo yatachochea shughuli za uchumi.

Baraza la Madiwani limepitisha  rasimu ya bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 hivyo  limehitimsha mchakato wa rasimu hiyo na kusubiria Baraka za Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.