• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

B’hango awafunda Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi katika kikao kazi kilichofanyika Machi 9, 2020 ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Posted on: March 9th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amewaagiza Wajumbe wa Mamlaka ya Mji mdogo Kiomboi kupanda miti ya matunda katika maeneo yao ya utawala.

Agizo hilo limetolewa leo Jumatatu machi 9, 2020 wakati akiongea na Wajumbe hao katika kikao kazi kilichofanyika  ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Ninawaagiza kuhakikisha azimio la Baraza la Madiwani kuhusu kupanda miti ya matunda linatimizwa na nyinyi wajumbe wa Mamlaka ya mji mdogo kiomboi ili kuupamba mji  ukae vizuri,” ameagiza Mwageni

Akiwajengea uwezo Wajumbe wa Mamlaka ya Mji mdogo Kiomboi,  Afisa Utumishi wa Halmashauri hiyo, B’hango Lyangwa amewaambia kuwa wanatakiwa kuhakikisha kipindi cha uongozi wao wanapata uwekezaji wakutosha huku akiwataka kufahamu kuwa kulitekeleza hilo nikuingia katika historia ya kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi.

Pia amewataka kufahamu kuwa uwepo wa wenyeviti wa vitongoji imara ndio utakosababisha Mamlaka hiyo kupata maendeleo.

“ Ninaomba mtambue kuwa mkiwa na ari ya maendeleo  na wananchi walio katika maeneo yenu watapata maendeleo,” amesema Lyangwa na kuongeza

 

“Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi haiji kufuta vitu vizuri ispokuwa inakuja kuviimarisha,”

Halikadhalika amewataka wajumbe hao kuifahamu mipaka ya maeneo yao itakayowawezesha kutekeleza majukumu ya kudumisha na kuimarisha amani na utulivu, kuendeleza uchumi endelevu na kuwashauri wakazi waliopo ndani ya maeneo yao, kuanzisha mipango miji kwa maendeleo ya maeneo yao, kuhamasisha jamii kupambana dhidi ya adui maradhi, ujinga na umasikini, kutunga sheria ndogo, kutoa kodi na  kutoza ushuru na garama mbalimbali.

Naye Afisa Mipango Miji wa Halmashauri hiyo, Valerian Msigala amewataka Wajumbe hao kufahamu kuwa ardhi hupanda thamani katika Mamlaka ya Mji mdogo, hivyo wanapaswa kutambua maeneo watakayo yauza yamepangiwa mpango gani katika mpango mji ili kuepusha migogoro.

“  Niwaondoe hofu kuwa huko tunakoelekea ni pazuri kuliko tulipotoka,” amesisitiza Msigala

Kwa upande wake mjumbe wa Mamlaka ya Mji mdogo Kiomboi, Enock Duke ameushauri uongozi wa Halmashauri hiyo kufikisha elimu walioipata kwa wananchi ili kuwarahisishia wajumbe hao utekelezaji wa majukumu yao mjini hapa.

Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi ilitangazwa na Tangazo la Serikali Na, 301 la Agasti 22, 2014.

MWISHO

Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi wakijadili muundo na kazi za wajumbe wa Mamlaka hiyo. Picha na Hemedi Munga

Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi wakiwasilisha muundo na kazi za Mamlaka hiyo. Picha na Hemedi Munga

Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kiomboi wakifuatilia mada zinazohusu kazi na muundo wa Mamlaka hiyo. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.