• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Bilioni 38.47 kuinufaisha Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kipindi cha 2020/2021

Posted on: January 24th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Baraza maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida limepitisha rasimu ya bajeti ya kiasi cha  zaidi ya shilingi Bilioni 38.6 kwa mwaka wa fedha  mwaka 2020 / 2021.

Baraza hilo limepitisha rasimu hiyo leo Ijumaa Januari 24, 2020 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

Jumla ya  Tsh38.47 bilioni zimepitishwa kutoka serikali kuu, Wadau mbalimbali wa Maendeleo na Makusanyo ya Halmashauri ambayo yamekadiriwa kukusanywa na kutumiwa kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Rasimu hiyo imeongezeka kwa mwaka wa fedha 2020/2021ukilinganisha na bajeti iliyopitishwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ambapo  Tsh27.15 bilioni zilikadiriwa kukusanywa na kutumika toka serikali kuu, Wadau wa Maendeleo na Makusanyo ya Halmashauri. 

 

Awali akiwasilisha rasimu hiyo  Kaimu Afisa Mipango, wa Halmashauri hiyo Emmanuel Migunga  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmahauri hiyo, Linno Mwageni amesema  katika fedha hizo  bilioni Tsh32,755,926,000 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi , bilioni 2,099,859,499 kwa ajili ya uendeshaji wa ofisi, bilioni 3, 658,801,592 miradi ya maendeleo na milioni 110,000,000 kwa ajili ya michango ya jamii.

 

Halmashauri hiyo ipo kwenye mwaka wa watano wa kutekeleza mpango mkakati  kwa kipindi cha miaka mitano ya awali ya utawala wa awamu ya tano ulioanzia mwaka 2015/2016 hadi mwaka 2020/2021.

‘’ Maandalizi ya mpango huo yamezingatia mpango wa maendeleo wa Dunia, mpango wa maendeleo wa Taifa wa miaka mitano, Ilani ya uchaguzi Mkuu ya Chama Cha Mapinduzi  ya mwaka 2015, Muongozo wa bajeti toka Wizara ya fedha, Muongozo wa Wizara ya TAMISEMI, Maelekezo ya Mkoa, Maelekezo ya Wizara mbalimbali kama Kilimo, Maji, Elimu, Afya, Utumishi na  Mifugo. ’’ amesema Migunga

‘’Mpango huo umejikita kutekeleza dira ya Halmashauri kuwa  na jamii yenye maisha bora na maendeleo endelevu na kutimiza dhima ya kutoa huduma bora kwa jamii kwa kutumia vizuri rasilimali, kujenga uwezo na utawala wa kisheria ili kuwa na maisha bora’’amesema.

 

 Migunga amesema katika taarifa hiyo kuwa Halmashauri hiyo inahakikisha  malengo ya  kupambana na janga la ukimwi, kutekeleza mkakati wa Kitaifa wa kupambana na rushwa, kuboresha utoaji na upatikanaji wa huduma za kijamii na kiuchumi vinatimia.

Pia kuongeza idadi na ubora wa huduma za jamii na miundombinu, kusimamia utawala bora wa kisheria,

kuboresha ustawi wa jamii, jinsia na uwezweshwaji  wa jamii, kukabiliana na dharura na maafa ili  kuwezesha jamii kushirikiana katika kupanga na kutekeleza vipaumbele vyake na kuboresha masuala ya Lishe hasa kwa watoto umri chini ya miaka mitano.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Simion Tyosela amewahimiza Madiwani kusimamia mapato ili kuipeleka Halmashauri katika muelekeo unaotakiwa kusimamia shughuli za maendeleo.

Pia  itasababisha huduma za kijamii kupitia mapato ya ndani kuweza kupatikana kila kata.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni ametoa taarifa kwa Madiwani wa Halmashauri hiyo kuhusu fedha iliyototewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama kwa muda kuwasalimia wananchi wa Shelui na kuwaunga mkono kwa  kutoa kiasi cha Tsh milioni 250 za kituo cha Afya cha kata hiyo, lakini badala yake ametoa shilingi milioni 400.

Mwageni alimshukuru Rais Magufuli kwa kuwajali wananchi wake kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya huduma ya Afya hivyo aliwasihi Madiwani hao kumuunga mkono kusimamia miundombinu inayotolewa na serikali ili wananchi wapate huduma stahiki.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                      

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela amewahimiza Madiwani kusimamia mapato yatakayoiwezesha Halmashuri kwenda katika muelekeo unaotakiwa wa kusimamia shughuli za maendeleo. Kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Samwel Shillah na Kulia mwa Mwenyekiti ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni. Picha na Hemedi Munga                                                                                                              

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amewaambia Madiwani kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameleta Tsh400 milioni kwa  ajili ya kituo cha Afya Shelui na TAMISEMI imewapatia POS 43 (point of Sel) za kukusanyia mapato. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                          

Baadhi ya Wakuu wa Idara mbalimbali wakifuatilia upitishaji wa  rasimu ya mpango wa kati na makisio ya bajeti ya mwaka 2020 hadi 2021. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.