• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Bilioni 7.6 zawezesha utafutaji na uchorongaji wa visima vitatu vya mafuta na gesi asilia katika kijiji cha Luono Bonde la Eyasi Wembere Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Posted on: July 25th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

Ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Waziri wa Nishati, Dkt, Medard Kalemani amerasimisha tukio la kwanza la uchorangaji kwa ajili ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini.

Dkt, Kalemani amelifanya zoezi hilo mwishoni mwa wiki hii wakati alipofanya ziara katika Bonde la Eyasi Wembere kijiji cha Luono  Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

“Sasa tunaanza safari ya kwenda kupata mafuta ambapo kwa hatua tuliyofikia inatoa matumaini kuwa tunayo miaka miwili toka sasa tunaweza kugundua mafuta ambayo ni neema kubwa sana,” amesema Dkt, Kalemani na kuongeza kuwa

“Shughuli za utafiti wa mafuta zinaendelea katika maeneo mengine ya Tanga kasikazini, Ziwa Tanganyika, Ziwa Rukwa na Bonde la Eyasi Wembere ambapo eneo hili la Wembere limeonesha kwa hatua ya haraka uwepo wa mafuta ya kuchimba.

Katika hatua hiyo amempongeza Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli katika awamu yake imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya utafutaji na uchorongaji wa mafuta na gesi asilia Tanzania.

“Ndugu zangu tambueni kuwa mwaka jana tulitenga fedha kwa ajili ya utafutaji na uchorongaji wa kuelekea kuchimba mafuta takribani dola 500milioni serikali imetoa” amesema na kutolea taarifa kuwa

“Kwa sasa tunamafuta yaliopo chini bado hayajakuja juu, hivyo tunaendelea kuyatafuta ili tuyatumie na kilichokuja juu ni gesi asilia ambayo tayari tunayo takribani 57.5 trilioni za gesi,”

Amefafanua kuwa tukio hilo la uchorongaji katika Bonde la Eyasi Wembere ni tukio kubwa kwa kuwa ndio tukio la kwanza la uchorongaji na utafutaji wa mafuta Nchini, hivyo ni bahati kwa wananachi wa Luono na Iramba kushuhudia  tukio kubwa ambalo halijawahi fanyika sehemu yoyote Tanzania.

Akitoa taarifa fupi ya utafutaji na uchorongaji wa mafuta na gesi asilia katika Bonde la Eyasi Wembere Nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mafuta la Taifa TPDC, Dkt. Vames Mataragio amesema kuwa wanalo jukumu la utafuatiji, uendelezaji na usambazaji wa mafuta na gesi.

“Mhe, Waziri tayari tumechimba visima 3 vyenye umbali wa mita 300 kwa lengo la kupata miamba tabaka yenye mafuta ilivyoenea ili kuweza kupata mafuta na gesi asilia,” amesema Dkt, Mataragio

Pia ameongeza kuwa wanaona upo uwezekano mkubwa wa kuwa na mafuta na gesi asilia kwa sababu jirani zetu Kenya na Uganda tayari wameisha pata mafuta katika maeneo ambayo yanafanana kabisa na maeneo ya Bonde la Eyasi Wembere.

“Mhe, Waziri hadi kufikia hapa tumeishatumia 7.6 bilioni katika utafiti ambapo 7.3bilioni zilitumika katika uchukuaji wa data kwa kutumia ndege huku 300milioni zikitumika kuchoronga visima vitatu,” amefafanua Dkt, Mataragio

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewashukuru wananchi wa Luono wa Bonde la Eyasi Wembere kwa kudumisha ushirikiano na usalama wa Uchorongaji na utafutaji wa mafuta na gesi asilia kwani mafuta yakipatikana yataweza kuwanufaisha wananchi wa Luono, Iramba, Singida na Tanzania kwa ujumla.

Naye Mkazi wa Kijiji cha Luono, Emmanuel Gedenga ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta mradi huo katika Kijiji cha Luona kwa sababu ikiwa mafuta yatapatikana wataweza kupata ajira za kutosha na kukifanya kijiji chao kuwa kama Ulaya.

Ufuatiliaji wa mafuta katika Bonde la Eyasi Wembere ulianza mnamo mwaka 2015/2016 kwa TPDC kufuatilia taarifa za awali za Kijiofizia za Nguvu za Uvutano na Usumaku ambazo zilionesha uwepo wa kina kirefu cha miamba tabaka yenye kuzalisha mafuta na gesi asilia.

MWISHO

Mhandisi Koleta Selsi akitoa maalezo ya hatua ya uchorongaji wa visima vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia ilipofikia mbele ya Waziri wa Nishati, Medard Kalemani alipofanya ziara katika kijiji cha Luono Bonde la Eyasi Wembere julai 23, 2020. Picha na Hemedi Munga

Mtambo unaotumika kuchorongea visima vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia Kijiji cha Luono Bonde la Eyasi Wembere Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Huo ndio Mtambo unaotumika kuchorongea visima vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia Kijiji cha Luono Bonde la Eyasi Wembere Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya miamba tabaka iliyotoka katika visima vitatu vilivyochimbwa Kijiji cha Luono Bonde la Eyasi Wembere tayari kwa kupelekwa maabara kubaini uwepo wa mafuta na gesi asilia katika eneo hilo. Picha na Hemedi Munga

Waziri wa Nishati, Medard Kalemani akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa TPDC. Kulia mwa Waziri huyo ni  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Zainab Said na Kushoto mwa Waziri huyo ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula. Picha na Hemedi Munga

Waziri wa Nishati, Medard Kalemani akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa TPDC. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.