• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Bishop Robert Kijanga akiombea barabara itokayo Singida kwenda Jijini Mwanza eneo la Kizonzo kata ya Shelui Wilayani Iramba panapotokea ajali za mara kwa mara.

Posted on: April 3rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Bishop Robert Kijanga wa kanisa la Evangelistic Assemblies of God Mjini Kiomboi amewaongoza Wachungaji katika maombi ya kupunguza ajali maeneo ya Kizonzo na Mgongoro yaliopo barabara kuu itokayo Singida kuelekea Jijini Mwanza.

Maombi hayo yamefanyika leo Ijumaa Aprili 3, 2020 katika maeneo tofauti tofauti ya barabara hiyo kuanzia Mgongoro hadi eneo la daraja la Sekenke chini ya Mlima Sekenke.

Akiongea katika maombi hayo, Bishop Kijanga amesema kuwa barabara hiyo imetengenezwa ili watu wapitishe mizigo ya biaashara, kurahisisha usafiri  na sio barabara ya mauti au kufanyiwa ibada za kishetani.

“ Mungu anayo haki ya kushinda, hivyo nia yetu ni kuvunja roho, mkuu wa anga atoae roho za watu mahala hapa, kuvunja nguvu za giza na vile vyote vinavyoingilia maisha na kuharibu mfumo wa binaadam,” amesema Bishop Kijanga na kuongeza

 

“ Tunamuomba Mungu kuleta usalama na amani katika barabara hiyo, kijiji cha kizonzo, kijiji cha Mgongoro na abiria wote wapitao katika barabara hiyo.”

Halikadhalika, amesema kuwa maandiko matakatifu yamesema kuwa mchawi hapaswi kuishi haswa anapokataa maandiko matakatifu yasemayo kuwa ombeni mtapewa, tafuteni mtaona, bisheni mtafunguliwa na andiko lisemalo niite nami nitaitika nami nitakuonesha mambo makubwa magumu usiyoyajua na maandiko mengineyo.

Kwa upande wake Mchungaji Robert Lugiko ameombea maeneo hayo  kuvunja nguvu za kichawi na nguvu za giza ili pawe salama.

“ Na tunakwenda kukomesha ajali katika eneo hili, kufuta jini na ajenti mkuu kutoka kuzimu mwenye kuangamiza roho za wanaadamu,” ameomba Lugiko

Mchungaji kutoka kitukutu, Yona Kidavya ameombea vyombo vya moto na madereva wake waepukane na vituko mbalimbali vya barabarani huku akikemea aina yoyote ya vitu vinavyoonekana na visivyoonekana vinavyosababisha utokeaji wa ajali.

 

Naye Afisa Tarafa wa Tarafa ya Shelui wa Wilaya hiyo, Nicholas Makoye amewashukuru Wachungaji hao kwa maombi ambayo huenda Mungu akanusuru roho za watu zinazopotea katika maeneo hayo kutokana na ajali za mara kwa mara.

Akitoa ushuhuda  mmoja wa  wakazi wa Kizonzo katika maombi hayo, Nkumbi Temwa amesema kuwa kutokana na yanayo zungumzwa na Madereva mbalimbali kuwa maeneo hayo hujitokeza mwanamke ambaye hajulikani maeneo anayoishi na punde baada ya kutoweka hutokea ajali.

“Hapa kuna pepo limeanza kusumbua na kusababisha ajali na huonekana binti ambaye hajulikani anakaa wapi na hafahamiki sura yake,” amesema Temwa

Naye mchungaji Samwel Majuta amesema kuwa wanaamini kuwa maombi walioyaomba Mungu ameyasikia na bila shaka atawajibu, hivyo ajali zote zitakoma katika maeneo hayo.

Maombi hayo yamefanyika kufuatia ajali iliyotokea wiki iliyopita ya lori lenye usajili namba T939 CBW lilipokuwa linalipita gari dogo (overtaking) na kugongana uso kwa uso na basi la MJ Safari lenye usajili namba T779 AWJ.

Kufuatia ajali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula alipotembelea eneo la ajali aliahidi kupeleka timu ya maombi kuombea kutokomeza ajali hizo.

Timu hiyo ya maombi, im emetembelea na kuomba takriban 38 kilometa za barabara hiyo kuanzia Malendi mpakani mwa Mkoa wa Singida na Tabora, Kizonzo, Shelui, Sekenke na  Misigiri.

Maombi hayo yamejikita kuombea kuvunja roho zilizokalia Kizonzo na Mgogoro, kuombea madereva wote kuendesha vizuri kwa kuzingatia taratibu za barabara,  kuombea barabara na mipaka yake kuwa salama, kuombea abiria wote wanaopanda magari kuwa salama, kuombea vyombo vya moto na kuombea Serikali ya Wilaya ya Iramba na Wasimamizi wa miundombinu ya Barabara.

MWISHO

Bishop Robert Kijanga akiombea barabara itokayo Singida kwenda Jijini Mwanza eneo la mpakani kati ya Wilaya ya Iramba na Igunga. Picha na Hemedi Munga

Mchungaji Samwel Majuta akiombea barabara itokayo Singida kuelekea Jijini Mwanza eneo la Kizonzo Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mchungaji Yona Kidavya akiombea barabara itokayo Singida kuelekea Jijini Mwanza eneo la Malendi mpakani mwa Mkoa wa Singida na Tabora. Picha na Hemedi Munga

Afisa Tarafa wa Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba, Nicholas Makoye  akiwashukuru Wachungaji kwa maombi waliyoyaomba kwenye barabara itokayo Singida kuelekea Jijini Mwanza eneo la Malendi mpakani mwa Mkoa wa Singida na  Tabora. Picha na Hemedi Munga

Bishop Robert Kijanga akiwa na wachungaji mbalimbali wakiombea barabara itokayo Singida kwenda Jijini Mwanza eneo la Kibigiri kata ya Shelui Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Bishop Robert Kijanga akiwa na wachungaji mbalimbali wakiombea barabara itokayo Singida kwenda Jijini Mwanza eneo la daraja la sekenke chini ya Mlima wa Sekenke Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.