• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC IRAMBA AIOMBA TARI KUSAIDIA WAKULIMA WILAYANI HUMO

Posted on: October 6th, 2021


Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Mhe. Suleiman Yussuf Mwenda ameiomba Wizara ya Kilimo kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kuendelea kutoa mafunzo ya kilimo hususani kanuni za kilimo bora kwa maafisa ugani na wakulima wilayani humo ili kuboresha kilimo na kuongeza tija katika mazao ya kilimo.

Mhe. Mwenda alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimo (2021/2022) Kiomboi Wilayani Iramba Mkoani Singida ambapo wadau mbalimbali wa kilimo walishiriki katika uzinduzi huo wakiwemo Wizara ya Kilimo, Wakulima , Maafisa Ugani, Taasisi binafsi na za Serikali (TARI, NMB, Shirika la Posta, TANESCO, Bodi ya Pamba, Feed the future, Action Against Hunger, Bio Sustain, Reliance Group, ETG) pamoja na Makampuni ya mbegu (SUBA-Agro, DK, SeedCo, Kibo Seed).

 Katika hotuba ya ufunguzi, Mheshimiwa Mwenda amesema TARI imekuwa ikitafiti mbegu bora za mazao mbalimbali na kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa maafisa ugani  na wakulima  hivyo kuitaka TARI kupeleka teknolojia hizo Wilayani Iramba ili wakulima waweze kunufaika kwa kulima kilimo chenye tija na kuachana na kilimo cha mazoea.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TARI aliyeshiriki katika uzinduzi huo Bibi Margaret Mchomvu alisema TARI imejipanga kupeleka teknolojia zilizoboreshwa Wilayani humo ikiwemo utoaji mafunzo kwa maafisa ugani na wakulima kupitia mashamba darasa ambayo yataandaliwa wakati wa msimu wa 2021/2022 hasa kwa zao la alizeti.

Bibi Mchomvu aliongeza kuwa TARI pia imepanga kuandaa maonyesho makubwa ya teknolojia zake zote katika mnyororo wa thamani kwa lengo la kubadilisha mtazamo, fikra na kutoa elimu kwa wadau wa kilimo hasa kwa  mazao ya alizeti, mahindi, mpunga, mtama, uwele, ulezi, pamba,mihogo, viazi vitamu, maharage na kunde. Mazao mengine ni ufuta, karanga, dengu, vitunguu na nyanya.

Nao baadhi ya Viongozi wa dini, Chama na Serikali walioshiriki katika uzinduzi huo wamewaomba wataalamu kilimo wawasaidie wakulima wilayani humo katika kuboresha  na kubadilisha kilimo chao ili kiwe na tija na Iramba iwe na mafanikio makubwa katika sekta ya kilimo.

Uzinduzi wa Msimu wa Kilimo Wilayani Iramba uliobebwa na kauli mbiu isemayo “Kilimo Iramba, Tija kwa kila mdau” ulifanyika Oktoba 6, 2021.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.