• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA AAGIZA USHIRIKI WA WAWEKEZAJI KATIKA MIRADI YA JAMII IRAMBA

Posted on: May 21st, 2025

DC MWENDA AAGIZA USHIRIKI WA WAWEKEZAJI KATIKA MIRADI YA JAMII IRAMBA


Iramba, Singida – Mei 21, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda, ametoa agizo kwa serikali ya kijiji cha Nkokilangi kuhakikisha kuwa wawekezaji wote wanaofanya shughuli za uchimbaji wa madini katika eneo hilo wanashiriki kikamilifu kwenye programu za kurudisha kwa jamii (CSR), ili kuhakikisha kuwa wananchi wananufaika moja kwa moja na uwekezaji unaofanyika kwenye ardhi yao.


DC Mwenda aliyasema hayo leo alipokutana na wachimbaji wadogo wa madini katika kijiji cha Nkokilangi, kata ya Ntwike, kitongoji cha Kibululu Matanda. Lengo la kikao hicho likiwa ni kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wachimbaji hao katika utendaji wao wa kazi za kila siku.


Katika kikao hicho, Mwenda alisisitiza serikali ya kijiji kuhakikisha inasimamia ipasavyo utekelezaji wa majukumu ya wawekezaji kwa jamii.


“Hakikisheni wawekezaji wote wa ndani na nje wanashiriki programu ya kurudisha kwa jamii lakini pia hakikisheni wananchi wote wa eneo hili wanapata taarifa zote muhimu juu ya uwekezaji huo. Wakija watuachie alama, alikuja Sunshine hapa akatuachia darasa Moja pale shule ya Msingi Nkokilangi. Tumieni muongozo kufahamu nini kinatakiwa kifanyike kwenye Jamii kwa kuzingatia uhitaji wa Jamii kwa wakati huu.” alisisitiza DC Mwenda


Mmoja wa wanakijiji, Michael Juma, alitumia nafasi hiyo kuwasilisha ombi kwa Mkuu wa Wilaya akiomba kutengwa kwa eneo maalum la kiwanja cha michezo kijijini hapo. Ambapo, Alisema kuwa kiwanja hicho kitakuwa msaada mkubwa katika kuendeleza shughuli za michezo na kujenga afya na mshikamano kwa vijana wa eneo hilo.


Katika hatua nyingine, DC Mwenda aliwataka wanakijiji wa Nkokilangi kujiandaa kwa ajili ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru unaotarajiwa kufanya ziara Wilayani Iramba mwezi Julai 2025. Alisisitiza kuwa ni fursa ya kipekee kwa wananchi kuonyesha mshikamano na maendeleo ya Wilaya ya Iramba.


Tangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI KUJADILI NA KUPOKEA TAARIFA YA CAG MWAKA WA FEDHA 2023/2024 TAREHE 18, JUNI 2025 June 16, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI

    July 08, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 2025

    July 07, 2025
  • TRA IRAMBA YAVUKA MALENGO YA UKUSANYAJI KODI KWA ASILIMIA 130, YAWASHUKURU WALIPAKODI

    July 01, 2025
  • DC MWENDA AKABIDHI SPIKA KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII IRAMBA

    July 01, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.