DC MWENDA, AFANYA ZIARA KUKAGUA MRADI WA UMALIZIAJI WA ZAHANATI YA MSAI, UJENZI WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI WILAYANI IRAMBA
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda amefanya ziara Februari 28, 2025 Kukagua mradi wa umaliziaji wa wa Zahanati ya Msai iliyopo Kijiji cha Msai kata ya Mtoa Pamoja na ujenzi wa Shule za Msingi na Sekondari wilayani Iramba.
Katika ziara hiyo DC Mwenda amewaagiza wataalamu wanaosimamia mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Msai kufanya kazi kwa uharaka na Uadilifu ili kukamilisha mradi huo ndani ya muda uliopangwa na uanze kutoa huduma kwa wananchi ifikapo Juni 2025.
"Hakikisheni mnakwenda na kasi ili kuendana na muda wa ukamilishaji wa Zahanati hii, iishe kwa wakati ili wananchi waanze kupata huduma hapa ifikapo mwezi wa sita mwaka huu. Simamieni kwa uadilifu na ubora unaotakiwa." Amesema DC Mwenda.
Miradi ya shule iliyokayokaguliwa ni Ujenzi wa Shule mpya Kizega, Ujenzi wa Mabweni na vyumba vya Madarasa ya Kidato cha Tano Shule ya Sekondari Kizaga, Ujenzi wa Shule mpya ya sekondari Mtoa, Ujenzi wa Vyumba vitano vya Madarasa na matundu 6 ya Vyoo vya wanafunzi Shule ya Msingi Tyeme, Ujenzi wa Mabweni Mawili na vyumba Vinne vya Madarasa ya Kidato cha Tano Shule ya Sekondari Kinambeu.
Katika Ziara hiyo DC Mwenda ameambatana na Katibu Tawala Wilaya ya Iramba Bi. Bupe Mwakibete, Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya pamoja na Watalamu mbalimbali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.
KIOMBOI, IRAMBA
Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA
Simu: 026 - 2532253
Simu: 026 - 2533001
Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz
Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.