• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA AIPONGEZA HALMASHAURI YA IRAMBA ONGEZEKO LA BAJETI MAKISIO YA MAPATO YA NDANI YA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Posted on: February 14th, 2025

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Iramba kwa kupitisha bajeti ya makisio ya Mapato ya ndani ya kiasi cha Shilingi Bilioni 3.8 ikiwa ni ongezeko la bajeti hiyo ikililinganishwa na makisio hayo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ya Shilingi Bilioni 1.9.


Mwenda ameyasema hayo Februari 14, 2025 katika Baraza Maalumu la Madiwani kupitia na kupitisha makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026.


“Wilaya yetu inayo mafanikio makubwa sana katika utekelezaji wa bajeti zilizopita, tangu nimefika hapa kumekuwa na ongezeko la bajeti yetu na wakati wote tumekuwa tukiitekeleza kwa mafanikio. Tumeikuta bajeti ya Shilingi Bilion 1.2, leo kwenye baraza hili imepitishwa bajeti ya Bilioni 3.8, haya ni mafanikio makubwa sana.” Amesema DC Mwenda


Katika hatua nyingine Mwenda ametoa pongezi kwa wilaya ya Iramba kwa kushika nafasi ya 8 ikiwa na asilimia 13 kati ya kati ya Halmashauri 10 zilizoongeza ufaulu mtihani wa darasa la saba kitaifa wa mwaka 2024.


Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Iramba likiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Innocent Msengi limepitisha Makisio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 ya kiasi cha Shilingi Bilioni 38.08.


Bajeti ya Maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 imewasilishwa na Afisa Mipango Bw. Fadhil Hassan kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri.


Amesema Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imekadiria kukusanya na kutumia Shilingi Bilioni 38.08 ambapo Ruzuku ya Mishahara Shilingi Bilioni 21.8, Ruzuku ya matumizi mengineyo Shilingi Bilioni 2.06, Mapato ya ndani shilingi Bilioni 3.8, Miradi ya Maendeleo 5.2 na Wahisani - Miradi ya maendeleo shilingi Bilioni 5.08.


Baraza la Madiwani limepongeza waandaaji wa Bajeti hiyo kwa kuzingatia vipaumbele mahususi vilivyowekwa Kwa ajili ya Maendeleo ya Halmashauri wakiamini Miradi ya Maendeleo itatekelezwa na Wananchi watapata huduma Stahiki.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.