• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC Mwenda akemea tabia ya kujichukulia sheria mkononi kudhuru watu Iramba

Posted on: April 6th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amekemea tabia ya kujichukulia sheria mkononi kudhuru watu pindi inapokuwa imetokea kutoelewana kwa wachimbaji wadogo wadogo wa madini ya dhahabu na badala yake wafuate sheria, taratibu na kanuni katika kutatua migogoro inayowakabili.

Mwenda ametoa kalipio hilo leo Jumanne Aprili 5, 2022 wakati alipokuwa akiongea na wachimbaji wa madini ya dhahabu katika mgondi wa Nabii Elia uliopo katika kijiji cha Misigiri kata ya Ulemo wilayani hapa.

“Ndugu zangu fahamuni kuwa jukumu langu lakwanza ni kuhakikisha hali ya usalama na amani kwa raia wote wilayani hapa.” Alisema

Aidha, aliwataka kuhafamu kuwa wao wametoka katika maeneo tofauti tofauti kuja kutafuta riziki katika mgodi huo, hivyo mgodi ukifungwa watapata shida katika kuendesha maisha yao.

Aliwaagiza wachimbaji hao kuwa na tabia ya kwenda polisi pale panapotokea mtu anatoa maneno ya kashfa, machafu na matusi ili polisi wamchukulie hatua na kuendelea nataraibu za kisheria.

“Hatuwezi kila mmoja awe anachukua sheria mkononi, kufanya hivyo ni kujiingiza katika makosa hata kama utakuwa ulichokozwa au haki ipo upande wako.” Alikataza

Kufuatia hali inayodaiwa kuwa baadhi ya viongozi na wachimbaji kupigana na kutiana majeraha, Mkuu huyo wa wilaya alikilani kitendo hicho nakuwataka wafahamu kuwa yeye akiwa Mkuu wa wilaya mwenye dhamana ya kulinda amani na usalama wa raia hajafurahia kitendo cha uvunjifu wa amani uliodaiwa kufanyika katika mgodi huo.

“Nakilani kitendo hichi, siridhiki na tabia hii, hivyo nawaasa ndugu zangu tufanye kazi hizi kwa kuzingatia na kuhesimu sheria, taratibu na kanuni ambazo serikali imeziweka.”

Akiongea na wachimbaji hao, Mkuu wa kituo cha Polisi kiliopo kata ya Ulemo wilayani hapa, Inspekta Alfred Mpimbwe aliwataka wachimbaji hao kuwa na nidhamu katika utendaji wa majukumu hayo na kufahamu kuwa pindi wanapokuwa wamepata fedha kutoka katika migao ya mawe yanayodhaniwa kuwa na dhahabu husababisha mji wa Misigiri kuchangamka.

Awali akitoa taarifa fupi ya namna ambavyo ugonvi ulivyotokea mmiliki wa mgodi huo, Nabii Elia alimuomba Mkuu huyo wa wilaya kupiga marufuku Shimwaa (pombe) ambayo imekuwa ikisababisha vijana hao kulewa na hivyo kupoteza nguvu na kuwa chanzo cha ugonvi kwa wachimbaji.

“Kwa kweli chanzo kikubwa cha kukomesha migogoro na ugonvi migodini ni kupiga marufuku Shimwaa ambayo imekuwa ikiharibu vijana ambao ndio tengemeo la kujenga uchumi wa nchi yetu.” Aliomba Elia

Hata hivyo, wachimbaji wa madini ya dhahabu katika mgodi huo walitoa ushauri wa namna ya kutatua migogoro inayodaiwa kutokea katika maeneo ya migodi.

Kwa upande wake mmoja wa wachimbaji katika mgodi wa Nabii Elia, Saimon Kindago alishauri kuwa mmiliki wa mgodi huo abadilishe viongozi ambao wanasimamia shughuli mbalimbali katika mgodi huo kwa sababu ndio ambao wanadaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo.

Naye Francis Emmanuel alishauri kuwepo kitengo cha ulinzi na usalama katika mgodi huo ili kuhakikisha katika maeneo yote ya mgodi yanakuwa salama na pale panapowezakutokea mgogoro au uvunjifu wa amani wanawakamata wahusika na kuwafikisha katika mkondo wa sheria.

Akiongea na Mwandishi wetu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Iramba, Dkt. Abel Mafuru alikiri kuwa mnamo Aprili 02 mwaka huu waliwapokewa majeruhi wawili ambao ni wakazi wa kijiji cha Misigiri wilayani hapa.

Dkt Mafuru alifafanua kuwa uchunguzi wa awali baada ya kuchukuliwa vipimo ulionesha kuwa Devison Samweli (56) alikuwa amevujika mfupa mkubwa wa mguu wake wa kulia na kuwa taratibu za kumpatia rufaa kwenda hospitali ya Mkoa wa Singida zinaendelea huku Peter Devis (37) akiwa amejeruhiwa katika paji lake la uso na kupata maumivu katika kifua chake.

Dkt Mafuru alithibitisha kuwa majeruhi hao hali zao zinaendelea vizuri.

Majeruhi hao wamedaiwa kupatikana kutokana na ugonvi ulioibuka katika mgodi wa Nabii Elia unaojishughulisha na kuchimba madini ya dhahabu.

Ilidaiwa kuwa chanzo kikubwa cha ugonvi huo ni ulevi uliopelekea wachimbaji hao kupigana baada ya kuchindwa kuelewana baada ya mchanga na mawe yanayodhaniwa kuwa yanadhahabu kupakiwa katika roli na kuonekana ujazo umezidi kiasi ukilinganisha na inavyokuwaga kwa ajili ya kuhamishwa kutoka duwara moja kwenda jingine.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.