• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC Mwenda amuagiza OCS kuwakamata wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo Iramba

Posted on: March 29th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

        

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amemuagiza Mkuu wa Polisi Tarafa ya Ndago INSP Rashidi Mchomvu kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria watu wanaowatishia amani watumishi waliopangiwa majukumu ya kusimamia miradi ya maendeleo.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Jumatatu Machi 28, 2022 wakati akiwa na Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Kamati ya Usalama wilaya kukagua miradi ya maendeleo katika kijiji cha Mwanduigembe wilayani hapa.

“Ninakupa wiki moja uhakikishe umewakamata watu wote wanaowatishia watumishi ambao wanatakiwa kusimamia miradi ya maendeleo ambao wanaogopa kudhuriwa na kuomba kuondoka katika kata ya Ndulungu na kuhamia kata nyingine.” Aliagiza

Aidha¸ aliongeza kuwa watu ambao wanaowatishia kuwadhuru watumishi wanatakiwa kufikishwa katika vyombo vya sheria ili watumishi hao waishi kwa amani na kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo kwa ajili ya manufaa ya wananchi.

Alieleza kuwa haiwezekani apatikane mtu ambaye anazuwia miradi ya serikali isitekelezwe na kuwatishia watu kutopata amani wakati mimi nipo kwa ajili ya kuhakikisha amani ipo kwa watu wote.

Pia, aliwataka mafundi kuongeza kasi ya ujenzi kwa sababu wananchi wanayahitajia majengo hayo kwa kiu kubwa.

Alisisitiza ubora wa majengo hayo kuwa sawa na kiwango cha fedha takiribani Tsh 600 milioni zilizotolewa na serikali.

Katika hatua nyingia, Mkuu huyo wa wilaya alimuagiza Afisa Elimu Sekondari, Godfrey Mwanjala kuhakikisha atakapomuandikia Katibu tawala Mkoa wa Singida kuhusu fedha iliyobakia kutenga bweni la wasichana na wananume.

Halikadhalika, aliwataka viongozi wanaosimamia miradi hiyo kufanya kazi zao kwa uwazi ili kila mmoja awe anafahamu namna ambavyo fedha hizo zinavyotumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Akiongea katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Iramba, Samwel Joel alieleza kuwa tayari watu wote wanaofanya wananchi wagome kujihusisha kikamilifu katika ujenzi wa miradi ya maendeleo wamekwishachukuliwa hatua stahiki.

“Sisi tumeishamaliza kazi hasa kwa viongozi wote wanaofanya wananchi wagome na kukwamisha miradi tumeishawachukulia hatua zinazostahiki na suala hili limekwisha” alifafanua

Awali akitoa taarifa fupi mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Afisa Elimu Sekondari, Godfrey Mwanjala alisema kuwa wanatarajia kujenga madarasa manane na kuokoa baadhi ya fedha ambazo zinawezakutumika kujenga nyumba za walimu.

“Mheshimiwa mkuu wa wilaya! naomba kutoa taarifa kuwa hivi sasa Mhandisi anaandaa BOQ ya fedha ambazo tumeziokoa kwa ajili ya kujenga nyumba ya walimu baada ya kuomba kibali toka kwa Katibu Mkuu TAMISEMI.” Alisema

Kwa upande wake mmoja wa mafundi wanaojenga majengo ya madarasa hayo, Marcel Jacobo alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea miradi ambayo imesaidia wao kupata ajira.

“Kwa kweli tunamshukuru Rais Samia na tunamuomba aendelee kuleta miradi mingine ili tupate ajira nakuweza kuendesha maisha yetu.”

Naye mmoja wa wanafunzi wa shule ya Sekondari Ndulungu, Swaumu Shila alimshukuru Rais Samia kwa kuwajengea shule kwani hapo awali hapakuwa na shule, hivyo walikuwa wakitembea umbali mrefu kuifuta shule ya Sekondari Mbelekese iliyopo katika kata ya jirani.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.