• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI 500 WILAYANI IRAMBA KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Posted on: December 8th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Mwenda Jumapili Disemba 8, 2024 amewaongoza Watumishi na wakazi wa kata ya Old Kiomboi kupanda miti katika Hospital ya Wilaya ya Iramba pamoja na Zahanati ya Tutu iliyopo kata ya Kiomboi wilayani humo, kuelekea maadhimisho ya kilele Cha miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara ambayo huadhimishwa Kila mwaka ifikapo Disemba 9.


DC Mwenda amesema Wilaya ya Iramba inasherekea maadhimisho hayo kwa kuwakumbusha Wananchi kuwa wanao wajibu wa kuhakikisha wanaienzi amani ili nchi iendelee kubaki salama na kushiriki shughuli za maendeleo popote pale walipo.


"Moja ya jambo kubwa ambalo Kama taifa tunatakiwa kulienzi ni namna ya kuboresha, kuitunza na kuiendeleza amani ya nchi yetu. Ni tunu kubwa ambayo tuko nayo Kama taifa ambapo wenzetu maeneo mengi tunu hiyo hawana... Tunaposherekea uhuru wa Taifa letu lazima tujue kwamba tunao wajibu kama wananchi wa kushiriki shughuli za maendeleo popote pale ulipo. Maendeleo ya mtu mmoja mmoja ndio maendeleo ya Taifa." Amesema Mhe. Mwenda.


Pia Mwenda amesema katika kipindi Cha miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania bara Serikali kwa kushirikiana na Wananchi yapo mengi ya kujivunia kimaendeleo katika sekta mbali mbali kichumi kijamii na kitamaduni ikiwa ni matoke ya kupiga hatua katika maendeleo ya nchi.


"Wakati huo Wilaya nzima kulikuwa na sehemu tatu tu za kupata huduma za afya...Leo hii tunazungumza Kila Kijiji Kuna Zahanati, Kila kata ina Sekondari. Tuna sahemu zaidi ya 54 ambazo zinatoa huduma za afya katika Wilaya hii. Amesema DC Mwenda


Aidha DC Mwenda ametoa wito kwa Wananchi kuendelea na zoezi la upandaji miti katika Msimu huu wa mvua na kuhakikisha miti hiyo inatunzwa ili iendelee kukua kubaki salama.


Jumla ya miti 500 ya kivuli, miti ya mbao pamoja na miti ya Matunda imepandwa, katika zoezi la upandaji miti lilofanyika mapema leo Asubuhi kwenye maeneo mbalimbali Wilayani Iramba . Halmashauri ya Wilaya ya Iramba inaendelea kutekeleza agizo la Serikali la kila Halmashauri kuhaksikisha inapanda miti milioni moja na laki tano (1,500,000).










Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.