• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA APONGEZA MRADI WA VISIMA KYALOSANGI, WAKULIMA KUNUFAIKA NA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

Posted on: February 4th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida,Suleiman Yusuph Mwenda, amepongeza utekelezaji wa mradi wa uchimbaji visima vya umwagiliaji katika Kijiji cha Kyalosangi, unaotekelezwa kupitia Mpango wa Mifumo Himilivu ya Chakula kwa kuzingatia matokeo (TFSRP-PforR). Mradi huu, unaosimamiwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa gharama ya Shilingi milioni 187.7, unatarajiwa kunufaisha wakulima wapatao 200.


Akizungumza Februari 4, 2025, wakati wa hafla ya kumkabidhi mkandarasi eneo la mradi huo, DC Mwenda alisisitiza kuwa visima hivyo vitakuwa chachu ya maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji, hasa katika uzalishaji wa mboga na mazao mengine yanayohitaji maji ya kutosha.


"Mradi huu ni neema kubwa kwa wananchi wa Kyalosangi na Wilaya nzima ya Iramba. Nawasihi wananchi kushirikiana na wataalamu ili kuhakikisha kilimo cha umwagiliaji kinatumika ipasavyo kwa maendeleo yenu," alisema Mwenda.


Pia aliishukuru Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji, akibainisha kuwa Wilaya ya Iramba ni miongoni mwa maeneo yanayonufaika na miradi hiyo katika Mkoa wa Singida.


"Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imeweka mkakati madhubuti wa kuboresha kilimo cha umwagiliaji. Hii inamaanisha kuwa sasa wakulima wa Iramba wataweza kulima mboga na mazao mengine kwa msimu wote wa mwaka, bila kutegemea mvua," aliongeza DC Mwenda.


Mradi huu ni moja kati ya miradi mikubwa ya kilimo cha umwagiliaji inayotekelezwa Singida, ikiwemo skimu ya umwagiliaji yenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 10, ambayo tayari inaendelea kujengwa. Miradi mingine itatekelezwa katika maeneo ya Kyengege, Ulemo, Mukulu, Old Kiomboi, na Mtoa.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.