• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA APONGEZA UJENZI WA KARAKANA YA UFUNDI SHULE YA MSINGI LULUMBA

Posted on: September 24th, 2025

DC MWENDA APONGEZA UJENZI WA KARAKANA YA UFUNDI SHULE YA MSINGI LULUMBA


Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda, amepongeza ukamilikaji wa ujenzi wa Jengo 1 la karakana ya ufundi na matundu 2 ya vyoo wenye thamani ya shilingi milioni 54 uliopo Shule ya Msingi Lulumba, wenye lengo la Kuwawezesha vijana wa miaka kati ya 14 hadi 19 kujiajiri wenyewe kwa fani za ufundi ambazo ni Ushoni, Kilimo cha bustani na ufundi magari.


Mwenda ameyasema hayo Septemba 23, 2025, wakati akikagua ujenzi wa mradi huo baada ya kupokea taarifa ya mradi kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Jacob Omary, DC Mwenda alisema "Mradi huu unalenga kuwajengea uwezo wa ufundi vijana kwa kujifunza na kuongeza kipato chao".


Aidha, alisisitiza wataalamu wa Halmashauri kuendelea kutoa elimu ya Mfumo wa NeST kwa mafundi ujenzi waliopo katika Kata ya Shelui ili waweze kushiriki kikamilifu katika zabuni za kazi za ujenzi zinazotolewa na Serikali.


“Tuna mafundi wengi katika kila kata, waiteni waambieni tunahitaji mafundi kwa sababu tunajenga shule hapa. Waelekezeni namna ya kuomba kazi hizi, waelezeni faida na waelekezeni jinsi ya kuomba kazi hizi kwenye mfumo ili waanze kuomba na kufanya kazi”


Katika ziara hiyo ya ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, DC Mwenda alitembelea na kukagua ujenzi wa Majengo ya Shule ya mkondo mmoja na madarasa 2 ya elimu ya awali katika shule ya msingi Shelui yenye thamani ya shilingi milioni 348.2, ujenzi wa madarasa 2 Shule ya msingi Galangala, ujenzi wa vyoo matundu 5, kichomea taka zahanati ya Maluga, ujenzi wa shule ya Sekondari ya Amali Kijji cha Kitukutu, ujenzi wa matundu matatu ya vyoo shule ya Msingi Ulemo, ujenzi wa nyumba ya walimu Shule ya Msingi Ntwike. Ziara hiyo ililenga kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO (WASIMAMIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA) October 23, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • KIKAO CHA KAMATI YA LISHE NGAZI YA HALMASHAURI KWA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA YA MWEZI JULAI HADI SEPTEMBA 2025 CHAFANYIKA

    October 20, 2025
  • KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 20, 2025
  • WAKAZI WA KIOMBOI WAENZI UTAMADUNI KUPITIA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 19, 2025
  • DAS MWAKIBETE ASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.