• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA ASITISHA MKATABA WA UCHIMBAJI MADINI USIO NA MASLAHI BAINA YA USHIRIKA WA UKOMBOZI NA KAMPUNI YA GREAT DRAGON CO.LTD

Posted on: March 12th, 2025

DC MWENDA ASITISHA MKATABA WA UCHIMBAJI MADINI USIO NA MASLAHI BAINA YA USHIRIKA WA UKOMBOZI NA KAMPUNI YA GREAT DRAGON CO.LTD.


Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda, amevunja mkataba kati ya kampuni ya uchimbaji madini Great Dragon Co. Ltd na wanachama wa Ushirika wa Ukombozi kutokana na mapungufu yaliyobainika katika mkataba huo.


Uamzi huo umefanyika Machi 12, 2025 kijiji Cha Nkonkilangi kata ya Ntwike wakati wa kikao kati ya wanachama wa Ushirika wa Ukombozi na mwekezaji wa Great Dragon Co. Ltd. ambapo ilibaininika kuwa baadhi ya wanachama waliingia mkataba kinyemela na mwekezaji huyo kwa lengo la kumkabidhi sehemu ya eneo la leseni wanayomilikiwa na chama hicho, bila ridhaa ya wanachama wote.


"Mkataba huu una mapungufu mengi sana, lazima tuhakikishe tunaingia mikataba kwa maslahi ya pande zote mbili ili pande zote zinufaike." Alisema DC Mwenda.


Pia, Mwenda amewataka wanachama wa Ushirika huo kuhakikisha wanaingia mikataba yenye manufaa kwa wote na kufuata ushauri wa wataalamu wa sheria wakati wote wanapofanya maamuzi ya kusaini mikataba.


"Mikataba tunayoiingia lazima ilinde maslahi ya Ushirika wetu. Kila jambo tunalofanya, ni lazima tushirikishe wataalamu wa sheria kwa msaada zaidi." alisisitiza DC Mwenda.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Ushirika huo, Samike Soli, alibainisha kuwa alipoingia madarakani Novemba 2024, alikuta baadhi ya wanachama wakiwa tayari wamesaini mkataba na Great Dragon Co. Ltd bila kufuata taratibu sahihi.


Naye Paulo Emanuel Ulaya mmoja wa wanachama wa Ushirika wa Ukombozi alieleza kuwa mkataba uliosainiwa haukuwa sawa na makubaliano ya awali ya wanachama.


"Tulikubaliana tumpe mwekezaji maduara matatu tu, lakini wenzetu waliingia mkataba wa eneo lote bila wanachama kufahamishwa." Alisema Paulo Ulaya.



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.