• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC Mwenda ataka wanaoajiri walinzi Wilayani Iramba wawe wametia mafunzo ya jeshi la akiba

Posted on: October 24th, 2021

Na Hemedi Munga

dediramba@singida.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amegiza makampuni yote yanayojishughulisha na ulinzi na usalama katika tasisi za serikali na binafsi waajiri askari ambao wamepata mafunzo ya jeshi la akiba.

Mwenda ameto agizo hilo leo Ijumaa Oktoba 22, 2021 wakati akiongea na askari walioko katika mafunzo ya jeshi la akiba Tarafa ya Kinampanda kata ya Ulemo Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Uwepo wa usalama na amani katika Wilaya hii una sababisha wananchi kujishughulisha na mambo ya maendeleo kwa utulivu unaowafikisha katika mafanikio wanayoyatarajia.

“Haiwezekani kuwapa silaha watu ambao wanakwenda kulinda ofisi aidha ya serikali au binafsi watu ambao hawana mafunzo ya jeshi la akiba.” Alikataza Mkuu huyo wa Wilaya na kuongeza kuwa

“Wale waajiri wote wanaojishughulisha kufanya kazi ya ulinzi katika Wilaya hii lazima wahakikishe askari wao wamepitia mafunzo ya jeshi la akiba ambao watakuwa na weledi wa kutunza silaha, nidhamu, heshima na wanajuwa uaminifu wa kuzitunza silaha hizo.”

Kufuatia hali hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito wa kuhakikisha kuwa makapuni ya ulinzi yanaajiri vijana ambao wametia mafunzo ya jeshi la akiba.

“Ni lazima tuwaajiri vijana hawa ambao wameonesha uvumilivu katika mafunzo yao ya jeshi la akiba na kamwe sinta kubali katika Wilaya yangu kuwaajiri watu wasio kuwa na mafunzo, hivyo ni lazima tutoe kipaombele kwa vijana walioshiriki mafunzo haya.”

Halikadhalika, Mkuu huyo wa Wilaya ametoa zawadi ya shilingi 100,000 kwa askari ambao wameonesha umakini wakupatia wakati wa kurenga shabaha.

Mshindi wa kwanza amepata shilingi 50,000, mshindi wa pili shilingi 30,000 na mshindi wa tatu shilingi 20,000.

Awali akitoa taarifa fupi ya mafunzo namna ambavyo askari hao wemeonesha umahiri na umakini, Staff Sagent  (SSGT) Benard kihaumbi amesema kuwa askari wa kiume (MG) Almasi Hamisi emekuwa wakwanza katika zoezi la kufunga na kufungua silaha huku askari wakike (MGM) wakionesha uhodari na ushindi wa kurenga shabaha.

Aidha Kihaumbi amemuhakikishia Mkuu huyo wa Wilaya kuwa askari hao wako makini, mahiri na wazima kuendelea na mafunzo yao.

“Ndugu Mkuu wa Wilaya nikuhakikishie kuwa askari hawa hakuna ambaye anaumwa, wako salama chini ya kamati ya kurenga shabaha yenye askari 13 inayoongozwa na Afande RG Matimiso.” Alisema SSGT Kihaumbi

Kwa upande mmoja wa askari hao, Almasi Hamisi amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuwatembelea kambini katika mafunzo na kuwapatia zawadi.

Hamisi alisema kuwa maagizo ya Mkuu huyo wa Wilaya yamewahakikishia kupata ajira punde badaa ya kumaliza mafunzo yao.

Kufuatia hali hiyo, Hamisi ametowa wito kwa vijana waliopo Wilayani Iramba kujiunga na mafunzo ya jeshi la akiba kwa sababu watapata weledi, ukakamavu, nidhamu na ajira itakayowawezesha kumudu maisha yao pamoja na kuiweka Wilaya yao katika hali ya usalama na amani muda wote.

Kwa upande Diwani wa kata ya Ulemo ambaye ni mmoja wa askari hao, Peter John amesema kuwa askari hao wanamorari na wameiva wako tayari kulitumikia Taifa.

Mafunzo hayo ya jeshi la akiba yalianza manamo mwezi wa saba 2021 na yako katika hatua za mwisho za kurenga shabaha.

MWISHO.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa jeshi waandamizi wanaoendesha mafuzo ya jeshi la akiba Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga.

Askari wa jeshi la akiba wakifuatilia maagizo ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda punde alipowatembelea kambini. Picha na Hemedi Munga

Askari wa jeshi la akiba wakifuatilia maagizo ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda punde alipowatembelea kambini Wakwanzan kushoto ni Diwani wa kata ya Ulemo, Piter J. Peter. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.