• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA ATOA ONYO KWA WATU BINAFSI WANAOUZA MBEGU ZA RUZUKU KWA WAKULIMA BEI TOFAUTI NA BEI ELEKEZI YA SERIKALI

Posted on: November 11th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda ametoa onyo kwa watu binafsi wanaouza mbegu za ruzuku kwa wakulima bei tofauti na bei elekezi inayotambuliwa na serikali.


Mwenda amebainisha hayo 11/11/ 2024 baada ya kutembelea duka la wakala (Ongeza Agrovet Iramba) anayeuza mbegu za ruzuku kwa wakulima kwa bei rasmi wilayani humo na kujionea zoezi la uuzaji mbegu za ruzuku linavyoendelea, huku akiwataka wakulima kuhakikisha wananunua mbegu kwa wakala aliyethibitishwa na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu (TOSCI).


“Lazima tuchukue tahadhari na ndio maana tunaelekeza ili wananchi wetu wasipate hasara, maana mwisho wa siku mtu atanunua ataenda kupanda hekali kadhaa hamna kitu atanufaika nacho, akitoka pale atakuwa na malalamiko kwa sababu amenunua mbegu bandia. Lakini Tukiwaelekeza kwenye vituo maalumu hivi maana yake hata sisi serikali tumejiridhisha kwamba hilo ni zao lenyewe halisi.” Amesema Mwenda


Aidha amewataka wakulima kuhakikisha wanahuisha taarifa zao kwenye mfumo kupitia kwa maafisa kilimo waliopo katika kata na vijiji vyao, ili kupata namba ya mkulima na taarifa hizo ziendane na uhitaji halisi wa kiwango cha mbegu wanazohitaji kulingana na ukubwa wa mashamba yatakayolimwa msimu huu.


Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya ya Iramba Bi. Marietha Kasongo amesema wanatekeleza agizo la Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha mbegu zote za mahindi zinaingia kwenye ruzuku.


“Tuna kaya 51,000 ambapo kila kaya angalau wanapaswa kulima ekari tatu, na zote zilimwe kwa kutumia mbegu bora na mbolea za ruzuku…kwa hiyo tunahitaji kilo 1,241,184 za mahindi ambazo ni mbegu bora” Alisema Kasongo.


Katika hatua nyingine Bi. Kasongo ameipongeza kampuni ya Ongeza Agrovet kwa kuendelea na usambazaji wa mbolea za ruzuku. Na amewaasa wakulima ambao bado hawajashiriki katika zoezi la upimaji wa afya ya udongo kuhakikisha wanashiriki zoezi hilo kupitia kwa maafisa kilimo.


Hatua hii inajiri wakati ambapo tayari msimu wa kilimo kwa mwaka 2024/2025 ukiwa umezinduliwa rasmi kimkoa novemba mosi mwaka huu wilayani Iramba.






Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.