• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA ATOA WITO KWA KILA MWANANCHI ALIYEJIANDIKISHA KUSHIRIKI KUPIGA KURA SIKU YA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

Posted on: October 23rd, 2025

DC MWENDA ATOA WITO KWA KILA MWANANCHI ALIYEJIANDIKISHA KUSHIRIKI KUPIGA KURA SIKU YA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025


IRAMBA, Oktoba 23, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda ametoa wito kwa wananchi walio jiandikisha katika Daftari la kudumu la wapiga kura Wilayani Iramba kwenda kupiga kura siku ya Uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 nchini.


Mwenda ameyasema hayo Oktoba 23, 2025 katika ukumbi wa shule ya Sekondari Shelui alipokuwa akizungumza na na viongozi wa Dini, viongozi wa kimila, wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji pamoja na wazee maarufu wa tarafa ya Shelui, ambapo alisisitiza umuhimu wa kupiga kura na kuendelea kudumisha amani.


“Twendeni tukahasishane kila mmoja kwa nafasi yake, tukawaambie watu tunawaongoza wote waliojiandikisha wakapige kura. Ukimaliza kupiga kura endelea na shughuli zako. Tuwahamasishe vijana kwamba twendeni tukalinde amani,” alisema DC Mwenda.


Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba Bi. Bupe Mwakibete amesema kupiga kura ni haki ya kila mwananchi kikatiba ili kumchagua Kiongozi anayeona anafaa kwa maendeleo endelevu na mwenye kudumisha amani.


Naye Mwenyekiti wa Kijiji Cha Nselembwe Said Tyuni amempongeza DC Mwenda kwa kuwatembelea viongozi hao huku akiahidi kuendelea kuwahamasisha Wananchi kijijini hapo kulinda amani.


DC Mwenda aliambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Wilaya katika mkutano huo.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SIKU YA UKIMWI DUNIANI DISEMBA 1,2025

    December 01, 2025
  • MAZOEZI YA VIUNGO YA KILA IJUMAA KWA WATUMISHI NA WANANCHI WOTE WA KIOMBOI NA MAENEO YA JIRANI

    November 27, 2025
  • RATIBA YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO KATA YA KASELYA

    November 25, 2025
  • DC MWENDA AWAPONGEZA WALIMU NA WANAFUNZI WILAYANI IRAMBA KWA MATOKEO MAZURI MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI

    November 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.