• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

Posted on: May 6th, 2025

DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI


Singida, Mei 6, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Yusuph Mwenda, amewahimiza walimu wa shule za msingi wilayani humo kufundisha kwa bidii madarasa yanayotarajia kufanya mitihani ya kitaifa, ili kuendeleza mwenendo chanya wa ufaulu wa wanafunzi katika wilaya hiyo.


Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa wilayani Iramba, Mwenda alisisitiza umuhimu wa kuendeleza mafanikio yaliyopatikana mwaka 2024 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ilishika nafasi ya 8 kitaifa katika shule zilizoongeza ufaulu wa darasa la saba nchini, ikiwa imeongeza ufaulu kwa asilimia13.


"Tunapaswa kuendeleza rekodi ya matokeo mazuri katika Wilaya yetu. Fundisheni kwa juhudi zote Madarasa yenye Mitihani ya Kitaifa ili mwaka huu pia tuendelee vunja rekodi ya kuongeza ufaulu pamoja na kupata matokeo mazuri." Amesema DC Mwenda


Katika ziara hiyo, DC Mwenda pia aliwapongeza wananchi wa Iramba kwa kujitolea nguvu kazi kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


“Nawapongeza sana wananchi wa Iramba kwa moyo wenu wa kujitolea. Katika kila eneo nililopitia, nimekuta mwitikio mkubwa wa wananchi kushiriki kwenye shughuli za maendeleo. Hili ni jambo la kupongezwa sana na kujivunia,” aliongeza DC Mwenda.


Katika ziara hiyo, DC Mwenda alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba ikiwemo: ujenzi wa ukamilishaji bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Kidaru (Thamani: Shilingi milioni 60), ujenzi wa matundu 10 ya vyoo Shule ya Msingi Kidaru (Shilingi milioni 17), ujenzi wa matundu 10 ya vyoo Shule ya Msingi Tyegelo (Shilingi milioni 17), ukamilishaji wa Kituo cha Afya Tyegelo (Shilingi milioni 150), ujenzi wa matundu 10 ya vyoo Shule ya Msingi Luono (Shilingi milioni 17), ujenzi wa Shule ya Msingi Nkokilangi (Shilingi milioni 250), ujenzi wa Zahanati ya Mseko (Shilingi milioni 250), mradi wa ufungaji wa mfumo wa gesi ya kupikia katika Shule ya Sekondari Shelui (Shilingi milioni 27.7).


DC Mwenda aliongozana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Wataalamu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.