• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC Mwenda awapongeza viongozi ukamilishaji kuweka vibao anwani za makazi Iramba

Posted on: May 1st, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz


Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewapongeza viongozi mbalimbali kwa hatua walioifikia ya ukamilishaji wakuweka vibao vya Anwani za Makazi katika taasisi, mitaa, barabara na nyumba.

Mwenda ametoa wito huo leo Jumamosi Aprili 30, 2022 alipofanya ziara ya kukagua ukamilishaji wa kuweka vibao vya Anwani za Makazi katika kila mtaa, barabara, nyumba na taasisi wilayani hapa.

“Kwa kweli hongereni sana kwa sababu kazi hii mnayoifanya inarizisha, hivyo hakikisheni wakati mnaendelea kuchonga vibao hivi mnachimba na mashimo kwa ajili ya kusimika nguzo za kuwekea vibao.” Alisema

Aidha, aliongeza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alitoa takribani Tsh 28 bilioni kwa ajili ya zoezi hili nchi nzima, hivyo fanyeni kazi mkijua kuwa kipo mtakachokipata.

Ninawashukuru sana na kuwaomba kuhakikisha kazi hii inakamilika kwa wakati kwa sababu swala hili lina tarehe ya mwisho ya ukamilishaji wake.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya aliwasisitiza viongozi hao kufanya manunuzi ambayo yanakuwa na risiti za mfumo wa kielektroniki.

Kwa upande wao mafundi waliopata tenda ya kutengeneza vibao hivyo wamekuwa na imani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuagiza swala ambalo limewapatia kipato na kufanikiwa kuendesha maisha yao.

Akiongea katika ukaguzi huo mmoja wa mafundi wanaochonga vibao hivyo, John Martin alisema kuwa Mfumo wa Anwani za Makazi umewafanya wao kutambulika na kuwa rahirisi kusafirisha samani mbalimbali wanazozitengeza katika mikoa na wilaya za jirani nchini.

“Kwa kweli ilikuwa ngumu kwa watu kufahamu siye mafundi tunapatikana wapi na tunaujuzi gani lakini kwa Mfumo wa Anwani za Makazi imekuwa rahisi siye kufahamika.” Alisema

Halikadhalika, alimpongeza Rais Samia kwa namna ambavyo aliagiza zoezi hili lifanyike ni maono ya hali ya juu ambayo yanafanikisha vijana kujipatia ajira za muda na zakudumu.

“Rais Samia ameturahisishia kupata wateja baada ya zoezi hili kuwepo tunafanya kazi kwa kujiamini na kutambua wateja wapo.”

Naye Alekzanda Martin alisema kuwa kazi hizi zimefanya wanaweza kukidhi mahitaji yao, hivyo alitoa wito kwa jamii kuendelea kuwaamini na kuwapa tenda zao.

Aliseama kuwa wao wanampongeza Rais Samia kwa sababu kama sioyeye kuagiza kutekeleza Mfumo wa Anwani za Makazi wasingepata riziki hiyo.

Aidha, wanamuomba Rais Samia kuwaangalia mafundi seremala kwa kuwapatia mashine zitakawasaidia kurahisisha utendaji kazi wao na kuzalisha samani kwa wingi.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.