• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

Posted on: March 10th, 2025

DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE


Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda amechangia madawati 28 Shule ya Msingi Msansao iliyopo kata ya Mtekente wakati wa ziara ya kamati ya Siasa Wilaya ya Iramba ilipotembelea shule hiyo Machi 10, 2025 kwa lengo la kujionea Mazingira ya utoaji wa Elimu shuleni hapo.


"Nachangia madawati 28 na nawapongeza sana kwa kuendelea kufanya vizuri katika Mtihani wa darasa la saba hongereni sana." Amesema DC Mwenda


Akiwasilisha taarifa ya shule ya Msingi Msansao kwa kamati ya Siasa Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bashiri Juma Makawia Ameeleza shule hiyo ina upungufu wa madawati 88 huku ikiwa imeendelea kufanya vizuri katika taaluma ambapo kwa upande wa mtihani wa kumaliza Elimu ya msingi, asilimia ya ufaulu imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka ambapo kwa miaka mitatu mfululizo ufaulu umepanda kutoka asilimia 25 ya mwaka 2021 hadi asilimia 74 mwaka 2024.


Kwa upande wake mbunge wa Iramba Magharibi ambaye pia ni Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba akiwakilishwa na Katibu wake Daud Madelu katika ziara hiyo amechangia jumla ya madawati 70 ili kukidhi uhitaji wa jumla ya madawati yanayohitajika kwa sasa shuleni hapo.


Katika ziara hiyo Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Iramba imetoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Masimba ambayo ujenzi wake tayari umeanza na unatarajiwa kuwanufaisha Wakulima zaidi ya 24000.


Pongezi hizo zimetolewa na Kamati hiyo inayongozwa na Mwenyekiti wake, Ndg. Samuel Joel Asher, wakati kamati hiyo ilipokagua na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa Wilayani Iramba.


Katika ziara hiyo, Kamati pia ilikagua miradi ya maendeleo ikiwemo Skimu ya Umwagiliaji Masimba, Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu (2 kwa 1) Shule ya Msingi Ushora Utemini yenye thamani ya Milioni 95 kupitia Programu ya GPE- TSP (Teachers Support Program), ambapo Hatua za Awali kwa ajili ya kuanza ujenzi zimeanza, Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Makunda kupitia Mradi wa Sequip kwa Gharama ya Milioni 544,225,626.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.