• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DED Iramba awafunda waliopata ajira za muda Mfumo wa Anwani za Makazi kuchunga mipaka ya kazi zao.

Posted on: March 16th, 2022

Na Hemedi Munga 

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Mhandisi Michael Matomora amewataka wakusanya taarifa na kuweka namba za Anwani za Makazi kuwa na uvumilivu na kutekeleza jukumu hilo kwa weledi na ufanisi wa hali ya juu.

Matomora ametoa wito huo leo Jumanne Machi 15, 2022 wakati akifungua mafunzo ya kutekeleza zoezi la Mfumo wa Anwani za Makazi katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Ninawaomba ndugu zanngu mkatumie maarifa yenu na kuchapa kazi kwa juhudi ya hali ya juu ili kutimiza jukumu hili la kitaifa.” Alisema Matomora

Aidha, amewataka vijana hao kutumia zoeli la Mfumo wa  Anwani za Makazi kujijenga katika maisha yao na  hasa wale ambao wanatarajia kupata  nafasi ya kuingia katika utumishi wa umma kwa sababu wao bado ni vijana.

Kufuatia uchaguzi uliofanyika katika usaili wao, wengi waliopatikana ni vijana wenye nguvu za kutekeleza jukumu hilo la kitaifa, hivyo Mkurugenzi huyo amewataka wale ambao wanatabia ya kutumia vinywaji vyenye kulewesha kuacha katika kipindi hichi ili kutekeleza zoezi hilo kwa weledi.

Halikadhalika, amewaomba kuweka akili zao ziwe makini katika kutekeleza zoezi la Mfumo wa Anwani za Makazi na kuwataka kuepuka mifarakano ya aina mbalimbali.

Pia amewaonya kuwa katika kipindi cha kutekeleza zoezi la Mfumo wa Anwani za Makazi kuacha kuanzisha mahusiano mapya ambayo yatapelekea sintofahamu na kuharibu zoezi hili la kitaifa.

“Niwaombe ndugu zangu kwa sababu mmekubali kufanya kazi hii ni wazi mmekuwa watumishi wa umma katika kipindi hichi cha kutekeleza jukumu hili la kitaifa, hivyo mnatakiwa kuwa na nidhamu ya kiutumishi.” Alisisitiza

Akiongea katika Mafunzo hayo, Mratibu wa Mfumo wa Anwani za Makazi wilayani Iramba, Valerian Msigala aliwataka wakusanya taarifa na kuweka namba za Anwani za Makazi kuwa makini katika kutekeleza zoezi hilo ili serikali iweze kufikia malengo ya kuimarisha upatikanaji, utoaji na upelekaji wa huduma na bidhaa mahali stahiki.

Aidha, aliongeza kuwa kukamilika kwa zoezi hili kutarahisisha biashara mtandao, kuimarisha ulinzi na usalama, kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kuongeza ajira na kuimarisha shughuli za utafiti na upatikanaji wa taarifa.

Kwa upande wake mtendaji wa Kata ya Nwike wilayani hapa, Ibrahimu Kingu aliwataka wananchi kufahamu kuwa zoezi la Mfumo wa Anwani za Makazi litafanyika punde baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo, hivyo waliunge mkono na kutoa taarifa pindi wakusanya taarifa na kuweka namba za Anwani za Makazi watakapofika katika maeneo yao.

“Natoa wito kwa wananchi wote wenye makazi katika wilaya hii kujiandaa na kulipokea zoezi hili muhimu ili kulifanikisha kwa manufaa ya Taifa letu,” Alitoa wito Kingu

Naye Bonifasi Ntui Mtendaji wa Kata ya Kidaru wilayani Iramba, alisema kuwa muitikio ni mkubwa na wananchi wanasubiri zoezi hili kwa hamu kubwa kwa sababu wamekuwa wakipata elimu ya Mfumo wa Anwani za Makazi kupitia vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii.

Ntui alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani kwa maono yake ya kutenga bajeti ya kutekeleza zoezi hili muhimu ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 hadi 2025.

“Ninaami kupitia mafunzo haya watendaji wa kata na wadau watakokwenda kutekeleza Mfumo wa Anwani za Makazi watakuwa mabalozi wazuri katika maeneo watakayopangiwa, hivyo jamii pia itakuwa na mtazamo chanya wa kutekeleza zoezi hili.” Alisema  

Zoezi za Mfumo wa Anwani za Makazi linaendelea katika wilaya na majiji nchini Tanzania.

Hatua hiyo inakuja ikiwa ni mwezi mmoja uliopita tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alipozindua oparesheni ya Mfumo wa Anwani za Makazi jijini Dodoma Februari 8, 2022.

MWISHO

Afisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Hemedi Munga akiwaelimisha watendaji wa kata, vijiji na wakusanya taarifa na kuweka namba za Mfumo wa Anwani za Makazi manufaa ya kakamilisha zoezi hilo katika ukimbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri hiyo leo Machi 15, 2022 mjini hapa. Picha na Brian Mambuya

Watendaji wa kata, vijiji na wakusanya taarifa na kuweka namba za Mfumo wa Anwani za Makazi wakisikiliza mada za Mfumo wa Anwani za Makazi katika ukimbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri hiyo leo Machi 15, 2022 mjini hapa. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.