• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Dkt, Medard Kalemani ametatua mgogoro wa UWAKESHE na Waziri kuwa Nguzo, Waya na Transfoma ni mali ya TANESKO na sio ya mtu binafsi.

Posted on: July 27th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Waziri wa Nishati, Dkt, Medard Kalemani amesikiliza na kutatua mgogoro wa Ushirika wa AWAKESHE na Muwekezaji aliyepeleka umeme katika kijiji cha Nkonkilangi kata ya Ntwike Wilayani Iramba.

Dkt Kalemani ametatua mgogoro huo leo Julai 23, 2020 wakati alipokuwa akiongea na wananchi hao katika ukumbi mdogo wa Halmashauri mjini hapa.

“Mgogoro huu ni mfupi sana kwa kuwa shughuli na rasilimali zote za kupeleka umeme kwa wananchi ni mali ya TANESCO na ndio jukumu la Serikali kupitia TANESCO  kuwapelekea umeme  wananchi wake,” amesema Dkt Kalemani na Kuongeza kuwa

“Serikali imekwisha toa maelekezo kuwa mwananchi yoyote hatakiwi kugharamia kifaa kimoja kimoja kama njia ya kupeleka umeme pale anapopeleka ispokuwa kulipia huduma tu na sio nguzo, waya au transifoma.”

Kwa kuwa huo ndio utaratibu wa Serikali kupitia Shirika la TANESCO kuhakikisha huduma ya umeme inawafikia wananchi na sio mwanachi kugharamia vifaa hivyo.

“Ndugu wananchi! utaratibu uliotumiwa na Bwana Hussein Waziri kupeleka umeme kwa wananchi na yeye kuwa kama dalali haliwezekani na haukubaliki .” amesisitiza

Hivyo, nitowe wito kwa TANESCO kukaa ili kupiga hesabu na gharama iliotumiwa na bwana Hussein ili kumlipa fedha zake kwa kuwa mita inayotumika ni ya kwake peke yake na hivyo kuwanyima wananchi uhuru wa kuwa na mita na matumizi ya umeme na Shirika kutopata mapato ya wateja wengi.

“Ndugu zangu fahamuni kuwa hakuna mtu mwenye mamlaka ya kumzuwia Mtanzania kutumia umeme anavyotaka kwa uhuru wake kwa kuwa  atakuwa amezingatia taratibu na jambo hilo linainyima TANESCO kupata mapato toka kwa wateja wengi,” amefafanua Dkt Kalemani na Kuongeza kuwa

“Maana anawanyima haki wananchi ya kupata umeme moja kwa moja toka Serikalini mpaka kwa sharti lake jambo ambalo halikubaliki, pia anainyima TANESCO kupata fursa ya kuongeza wateja jambo ambalo halikubaliki kwa sababu Shirika ni lazima litafute mapato kwa kuongeza idadi ya wateja kwa uhuru wao.”

Kufuatia changamoto hiyo Dkt Kalemani ameiagiza TANESCO kumrejeshea Bwana Hussein fedha zake na mitambo kubaki kuwa mali ya TANESCO.

“Niagize Wachimbaji wanaotaka umeme kujaza fomu ili waunganishiwe umeme wao wenyewe na utaratibu wa agizo hili uanze leo mara moja ili wananchi wawe wateja wa TANESCO na sio bwa Hussein,”

“Ninaomba nipate maelezo ya meneja wa TANESCO aliye ruhusu mfumo huu Desemba mwaka jana ili tuchukue hatua na iwe marufuku kwa TANESCO Wilaya, Mkoa au Makao Makuu kumilikisha umeme kwa mtu binafsi kwa lengo la watu binafsi kuwatumia watu wengi, hatuwezi kuwa na madalali wa umeme kwa watanzania wengine,” ameagiza Dkt Kalemani

Awali akiwasilisha taarifa fupi ya namna mgogoro ulivyotokea kati ya   chama cha Ushirika UWAKISHE na Mwekezaji Hussein, Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula amesema kuwa Wilaya haifurahi kuona kuwa mgogoro huu unaendelea kwa sababu unakwamisha uzalishaji.

“Kwa kweli Mhe, Waziri niliposikia unakuja nilifurahi sana maana tunajua tunapata hitimisho la mgogoro huu, ili shughuli za uzalishaji ziendelee” amesema Luhahula

Kwa upande wake mjumbe wa Ushirika wa UWAKESHE Konkilangi, Anjela Kahaya ameiomba Serikali kuwapelekea umeme katika maeneo yao ili kuwarahisishia uvutaji wa maji yanapokua yamezidi katika mashimo yanayochimbwa dhahabu.

Naye Mwakezaji wa umeme kijiji hicho, Waziri Hussein ameishukuru Serikali kwa uamuzi wake wa kusogeza nishati ya umeme katika maeneo hayo na kuahidi kuwa atashirikana na TANESCO kutekeleza agizo la Mhe, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.