• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

HAKIKISHENI WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA WANARIPOTI NA UANDIKISHAJI WA WATOTO WENYE UMRI WA KUANZA ELIMU YA AWALI NA DARASA LA KWANZA UNAKAMILIKA KWA WAKATI-DC MWENDA

Posted on: January 22nd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda amewataka Maafisa Watendaji Kata, Maafisa Elimu Kata na Walimu Wakuu Wilayani Iramba, kila mmoja ahakikishe Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza wanaripoti na uandikishaji wa watoto wote wenye umri wa kuanza Elimu ya Awali na Darasa la Kwanza unafanyika na kukamilika mapema ili kuwapa fursa walimu kuendelea kufundisha.


Dc Mwenda amesema hayo Jumatano Januari 22, 2025 wakati akipokea Taarifa ya Kuripoti kwa Wanafunzi wa kidato cha Kwanza na Uandikishaji wa Wanafunzi wa Elimu ya Awali na darasa la kwanza wakati akizungumza na Wakuu wa idara na Taasisi za Serikali,Watendaji wa Kata,Maafisa Tarafa na Watumishi wa Makao Makuu ya Halmashauri


Amesema Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023 inasisitiza utoaji wa elimu bora, kuanzia Elimu ya Awali ambayo ndiyo msingi wa kwanza katika mfumo wa Elimu rasmi kote ulimwenguni. Pia amesema tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa Elimu ya Awali ina mchango mkubwa katika makuzi na malezi ya mtoto kiakili, kimwili na kijamii.


Aidha, amesema, Serikali imeendelea kutekeleza mpango wa elimu bila ada kuanzia Elimu ya Awali hadi Kidato cha Sita.


"Hakikisheni wanafunzi wa kidato cha Kwanza wanaripoti bila kudaiwa mchango Wowote kwa kuwa Rais wetu anatoa Fedha kupitia Elimu Bure na ifanyike oparesheni itakayowahusisha Watendaji wa Kata na Vijiji Maafisa Elimu Kata,Walimu Wakuu na kuwakamata Wazazi wote watakaoshindwa kuwapeleka Watoto shuleni" Alisisitiza DC Mwenda


Ameongezea kwa kutoa wito kwa wazazi wote wenye wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari wahimizwe kuwapeleka shule wanafunzi hao mepama iwezekanavyo ili kuepuka kukosa mafunzo kabilishi (orientation course) yanayotolewa kama msingi wa ujifunzaji katika ngazi hiyo ya elimu.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.