• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Halmashauri ya Wilaya ya Iramba yangara tena maonesho ya Nane Nane mwaka huu.

Posted on: August 23rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni ametoa pongezi na kupokea  cheti cha ushindi wa Maonesho ya Nane Nane mwaka huu toka kwa wajasiriamali na wakulima walioshiriki maonesho hayo na kufanikiwa kupata ushindi ukilinganisha na Halmashauri sita na Manispaa moja za Mkoa wa Singida zilizoshiriki.

Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Nawapongeza sana kwa ushindi huu, hivyo Idara ya Kilimo iendelee kuwashawishi wakulima na wajasiriamali kujiandaa kwa maonesho yajao,” amepongeza Mwageni na kuongeza kuwa

“Kwa yule aliyebuni kifaa aina ya pawatila akiaswa kuongeza ubunifu ili awe na uwezo wa kuwa na mashine nzuri ya kusaga na kukoboa nafaka kwa ajili ya kusindika bidhaa na kuepuka kuuza mahindi gafi kwa sababu itakuwezesha kupata pumba na unga ambavyo vitakua na bei ya juu kibiashara,”

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo amemuahidi mbunifu huyo kumpatia mashine ya kuchomelea ili kuja kufanya kazi ya kutengeneza pawatila litakalokaa Halmashauri kama maonesho na kusaidia ubebaji wa taka ngumu katika maeneo mbalimbali ya mji wa kiomboi.

“Naomba ufahamu kuwa ukifanya kazi yenye viwango vizuri itakuwezesha kupata mtaji kupitia mikopo ya vijana inayotolewa na Halmashauri, kujiendeleza kiuchumi” amesema Mwageni

Wajasiriamali na Wakulima hao wameaswa kulitumia jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Iramba liliyopo katika viwanja vya Nzuguni Nane Nane kuwa ni fursa kwao kupeleka bidhaa mbalimbali ikiwemo mbogamboga, kambare, pelege na kamongo watokao ziwa Kitangiri na kutokusubiri wakati wa Nane Nane tu.

“Ni fursa kulitumia jengo hilo la kibiashara hasa kwa sababu lipo karibu na jengo la soko la Ndugai Jijini Dodoma, hivyo mtapata wateja tu,” ametilia mkazo Mwageni

  

Halikadhalika, amewataka wadau hao kwenda Nane Nane kwa ajili ya kutafuta na kutangaza soko la bidhaa wanazozalisha ili kujipatia wateja wakati wa Nane Nane na usio wa Nane Nane.

Mapema akitoa taarifa fupi mbele ya Mkurugenzi huyo Mwenyekiti wa Wajasiriamali na Wakulima hao, Flora Richard amesema kuwa wakulima na wafugaji wamefanikiwa kupata elimu ya juu ya teknolojia mbalimbali za kilimo, ufugaji na usindikaji.

Pia amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imefanikiwa kupata ushindi wa nafasi ya kwanza kimkoa na kutoa mkulima bora kwa nafasi ya kwanza kikanda katika maonesho yaliofanyika Nzuguni Jijini Dodoma mwaka huu.

Naye Mshindi wa zao la mahindi kanda ya Kati, toka Wilaya hiyo kata ya Kyengege Kijiji cha Mgundu,

Yesaya Njolle amesema kuwa wamejifunza kuwa kilimo kinauwezo wa kumtoa Mkulima katika umasikini na kwenda kwenye hali ya kati ya maisha.

Ameongeza kuwa kilimo cha kisasa kwa wakati wa masika na kile cha kiangazi ikiwa masharti yatafuatwa kwa kuzingatia maarifa na weledi walioupata wanaouwezo wakupata mazao msimu wa kipwa na masika.

MWISHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akipokea cheti cha ushindi wa maonesho ya Nane Nane mwaka huu toka kwa mweneyekiti wa Wakulima na Wajasiriamali walioshiriki maonesho hayo. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akionesha cheti cha ushindi wa maonesho ya Nane Nane mwaka huu toka kwa mweneyekiti wa Wakulima na Wajasiriamali walioshiriki maonesho hayo. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.