• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Hatimaye kituo cha Afya Ndago chazinduliwa na kuanza kutoa huduma ya upasuaji wa dharura. Picha na Hemedi Munga

Posted on: March 2nd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amezindua majengo mapya na huduma ya upasuaji wa dharura kituo cha Afya Ndago kilicho jengwa kwa fedha zilizoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Luhahula amezindua huduma hiyo leo Jumatatu Machi 2, 2020 katika kiwanja cha kituo cha Afya Ndago Wilayani Iramba Mkoa wa  Singida.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu huyo wa Wilaya, amewataka wananchi kuyalinda majengo hayo vizuri kwa kuwa ni kumbukumbu kubwa katika mji wa Ndago.

“ Niwaombe wananchi wote kuyalinda majengo haya kwa sababu ni mali yetu ili yaweze kudumu,” amesama Luhahula na kuongeza

“ Niwaombe Wataalamu na Madaktari  kuendelea kutoa huduma kwa weledi.”

Halikadhalika amewaomba Wananchi kujiunga na iCHF iliyoboreshwa ambayo inampa Mwanachi fursa ya kutibiwa hadi ngazi ya Mkoa kwa watu sita katika familia.

“Ndugu zangu hakikisheni mnajiunga na iCHF iliyoboreshwa na wala msisubiri muuguwe ndio  mwende mkachajiwe fedha maana kama mtu hana  iCHF iliyoboreshwa garama ni kubwa sana,” amesisitiza Luhahula

 

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Mfamasia wa Wilaya  Zuberi Abdallah amesema mradi umelenga kusogeza huduma za Afya hasa za dharura za uzazi kwa kinamama wajawazito, watoto na wananchi wote wa Tarafa ya Ndago.

Aidha ametumia fusra hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  kwa Kuleta Tshs400 milioni zilizotumika katika ujenzi wa majengo hayo.

Pia amebainisha mchango wa mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo na  fedha za wadau wa mfuko wa Afya wa pamoja (Performance Trenche) takribani Tshs61.52 milioni huku michango ya wananchi ikiwa ni  Tshs8 milioni.

Ujenzi na ukarabati wa majengo hayo wenye jumla ya takribani Tshs469.528 milioni kujenga jengo la mama na mtoto, nyumba ya mtumishi, jengo la kufulia (laundry), jengo la kuhifazia maiti (mortuary), jengo la maabara (laboratory) na jengo la upasuaji (Theater).

Awali kituo cha Afya Ndago kilikuwa na uwezo wa kutoa huduma ya wagonjwa wanje (OPD), huduma ya kulaza wagonjwa (IPD), huduma za maabara, huduma ya Afya ya uzazi na mtoto, huduma ya tiba na malezi kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi (CTC).

Aidha kukamilika kwa majengo hayo kumewezesha fursa ya kuanza rasmi upasuaji wa dharura, hivyo kufanikiwa kuondoa adha ya wagonjwa wanaotoka maeneo ya ndago na vitongoji vyake.

Naye Mwenyekiti wa Huduma za Jamii, Kinota Hamisi amewataka wananchi kuto ihujumu miundombinu hiyo huku akiwahakikishia kuwa serikali italeta vifaa tiba na waganga hivi karibuni.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Ndago, Henry Nkandi amewataka wananchi hao kutumia fusra ya kuanzisha biashara kwa kuwa Ndago itapokea watu wengi watakaokuwa wakihitaji huduma mbalimbali.

 

“ Ndugu zangu tambueni kuwa Tarafa ya Ndago inakata 6, hivyo watu wote watakuja Ndago kupata huduma za Afya na nyinginezo hivyo fungueni biashara zitakazowahudumia hao,” amesema Nkandi

Naye mmoja wa Wazazi aliojifungua katika kituo hicho jana ambaye hakutaka jina lake lifahamike ameishukuru serikali na Madaktari wanaotoa huduma hapo kwa huduma nzuri wanazozipata na kupunguziwa garama walizokuwa wakizitoa kwenda Hospitali ya Wilaya Mjini Kiomboi.

MWISHO

 

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kushoto, Hussein Sepoko akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba wakienda kukagua majengo mapya na huduma ya upasuaji wa dharura kituo cha Afya Ndago katika siku ya uzinduzi wa majengo na huduma hiyo. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amezindua majengo mapya na huduma ya upasuaji wa dharura kituo cha Afya Ndago kilicho jengwa kwa fedha zilizoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                          

Mfamasia wa Wilaya ya Iramba, Zuberi Abdallah akisoma taarifa ya Mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Ndago uliogarimu takribani Tshs469.528 milioni. Picha na Hemedi Munga                                         

Meneja wa Benki ya NMB mjini Kiomboi akiwaeleza wananchi waliohudhuria uzinduzi wa majengo mapya na huduma ya upasuaji wa dharura kituo cha Afya Ndago fursa zilizopo katika benki hiyo, ikiwa ni pamoja na  akaunti ya mtoto,ukopeshaji wa ujenzi wa nyumba na mkopo wa ujasiriamali. Picha na Hemedi Munga

Wananchi mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa  majengo mapya na huduma ya upasuaji wa dharura kituo cha Afya Ndago . Picha na Hemedi Munga                                                                                  

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela akiwashukuru wataalumu wa Afya na wote walioshiriki katika ujenzi wa majengo hayo tangu hatua ya awali mpaka kukamilika na kuzinduliwa. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                                                      

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula akimpokea mtoto aliozaliwa siku ya uzinduzi wa kituo cha Afya Ndago. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.