• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

IRAMBA YANUFAIKA NA HUDUMA YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA

Posted on: October 14th, 2025

IRAMBA YANUFAIKA NA HUDUMA YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA


Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ni miongoni mwa Halmashauri saba za Mkoa wa Singida zilizopokea huduma ya Madaktari Bingwa wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, waliotoa huduma za kibingwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiomboi kuanzia Oktoba 6 hadi 10, 2025.


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Oktoba 10, 2025 hospitalini hapo, Afisa Tawala Bi. Dorothy Mwangamila alitoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha programu hiyo, sambamba na kuwashukuru madaktari bingwa kwa kujitoa kutoa huduma hizo muhimu karibu na wananchi.


“Nianze kwa kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa programu hii. Nawashukuru pia kwa kujitoa kwenu kuja katika hospitali hii kutoa huduma hizi za kibingwa… Huduma hizi zimekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Iramba,” alisema Bi. Mwangamila.


Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Dkt. James Komanya, alisema kuwa mwezi Oktoba 2025 jumla ya wagonjwa 345 walipata matibabu kupitia programu hiyo ya Madaktari Bingwa, ikilinganishwa na wagonjwa 425 waliopatiwa huduma mwezi Mei mwaka huu.


Alibainisha kuwa kupungua kwa idadi hiyo kunatokana na huduma hizo kufanyika mara kwa mara wilayani Iramba, jambo linalowasaidia wananchi wengi kupata matibabu mapema na kwa urahisi zaidi.


Huduma hizo ni sehemu ya Programu Maalum ya Madaktari Bingwa wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inayotekelezwa katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini kwa lengo la kusogeza huduma za afya za kibingwa karibu na wananchi na kupunguza gharama za kusafiri kufuata huduma hizo mbali.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO (WASIMAMIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA) October 23, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • KIKAO CHA KAMATI YA LISHE NGAZI YA HALMASHAURI KWA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA YA MWEZI JULAI HADI SEPTEMBA 2025 CHAFANYIKA

    October 20, 2025
  • KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 20, 2025
  • WAKAZI WA KIOMBOI WAENZI UTAMADUNI KUPITIA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 19, 2025
  • DAS MWAKIBETE ASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 25, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.