• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

JUMLA YA Tsh. MILIONI 600 ZINATARAJIWA KUNUFAISHA VIJIJI 40 KATIKA MRADI WA UBORESHAJI USALAMA WA MILKI ZA ARDHI

Posted on: April 19th, 2024

Vijiji 40 Kati ya vijiji 70 Wilaya ya Iramba Mkoani Singida vinatarajiwa kunufaika na mradi wa uboreshaji na usalama wa milki za Ardhi ikiwemo upimaji mipaka, kutenga maeneo ya Malisho, Kilimo, Maeneo ya Taasisi za Serikali, ama upangaji na matumizi Bora ya ardhi ndani ya Vijiji hivyo na kupewa Milki za kimila, Lengo kuu ni kuondoa Migogoro ya Ardhi  iliyopo.

Hayo yamejiri Wakati wa mafunzo ya wadau wa ardhi yaliyoandaliwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mafunzo yaliyofanyika wilayani Iramba  na kufunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Yusuph Mwenda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Omary Dendego.

Katika hotuba yake kwa wadau hao ambao iliwahusisha  Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata,Viongozi wa Dini,Viongozi wa Kimila, Wafanyabiashara, Walemavu, Wakulima wakubwa na Wadogo pamoja na viongozi wa Taasisi za Serikali na Binafsi, Mkuu wa Wilaya Suleiman Mwenda anasema.

"Migogoro ya Ardhi ni Mingi katika Nchi yetu. Kwenye ziara ya Katibu Mwenezi Itikadi na Mafunzo  CCM, katika ripoti yake, Zaidi ya asilimia 70 ya kero alizozitatua ni migogoro ya Ardhi ; Hivyo ilimfanya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kugundua hili ni tatizo kubwa akakopa fedha Benki ya Dunia Dola Mil. 150 sawa na Bilioni 346, kwa ajili ya kupima na kutoa  Hati milki za Kimila zaidi ya Milioni 2 nchini na ndiyo maana na Iramba imenufaika na Mil. 600". Amesema Mwenda.

"Ni Imani yangu baada ya kukamilika kwa zoezi hili Migogoro ya Ardhi Iramba na kote nchini itakuwa imepungua kamasiyo kuisha kabisa ". Ameongeza DC Mwenda

Katika Vijiji 40 ambavyo vinanufaika na mradi huu Wilayani Iramba ni pamoja na  Kinalilya, Kisana, Kisimba, Kisiriri, Ulemo, Uwanza,Maluga,Galangala, Kyalosangi, Kisharita, Nguvumali, Mdonkolo, Zinziligi, Songambele, Luzilukulu, na Lunsanga.

Vingine ni Kisonga, Urughu, Kaselya, Nsonga, Kipuma, Ndulungu, Mwanduigembe, Mahola, Mang'ole, Mlandala,Masimba,Ujungu, Msai, Mtoa, Tintigulu, Wembere, Kibigiri, Mingela, Nsunsu, Luono,Ndurumo, Kidaru, Msansao na Tyegelo

Aidha Vijiji ambavyo  tayari Vimeshapimwa na Kuingia kwenye matumizi Bora ya Ardhi ni pamoja na Kisimba, Kisiriri, Kinalilya, Kisana, Kyalosangi, Uwanza, Kisharita, Galangala, Ulemo, Maluga, Zinziligi, Urughu, Kisonga, Kaselya, Luzilukulu, Lunsanga, Nguvumali, Nsonga, Songambele, na Mdonkolo Vijiji hivi Vimepitiwa kuanzia  Februari 10 2024 hadi April 17,2024.

Vijiji ambavyo Mradi umeendelea navyo ni  Kipuma, Ndulungu, Mwanduigembe, Mahola, Mang'ole, Mlandala, Masimba, Ujungu, Msai, Mtoa, Tintigulu, Wembere, Kibigiri, Mingela, Nsunsu, Luono, Ndurumo,Kidaru, Msansao na Tyegelo

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.