• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Emmanuel Makwaya amewataka wajasiriamali na wasindikaji wa mafuta kufahamu kua mafunzo hayo yakitekelezwa ni fursa muhimu inayochangia pato la Taifa, kuongeza ajira na kuondoa umasikini inchin

Posted on: February 20th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Shirika la viwango Tanzania (tbs) limeendesha Semina kwa wazalishaji na wasindikaji wa  bidhaa ya mafuta ya kula  wilayani Iramba.

Semina hiyo imefanyika leo Alhamisi Frebuari 20, 2020 Ukumbi Mdogo wa Halmsahuri  mjini hapa.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Emmanuel Makwaya amewataka wajasiriamali na wasindikaji wa  mafuta kufahamu kua mafunzo hayo yakitekelezwa ni fursa muhimu inayochangia pato la Taifa, kuongeza ajira na kuondoa umasikini inchini.

Mafunzo hayo yatawawezesha kuzalisha bidhaa zinazokidhi matakwa ya viwango na kuziongezea thamani bidhaa zinazozalishwa kupitia mfumo wa uthibitishaji ubora wa bithaa.

Kuyaingiza mafuzo hayo kivitendo kutaiwezesha serikali kufikia malengo ya Taifa ifikapo 2025 kua na uchumi wenye nguvu, imara na wenye ushindani.

Aidha Makwaya amewataka washiriki hao kuelewa lengo la mafunzo hayo kua ni kujipatia elimu juu ya viwango, uthibitishaji ubora wa bidhaa na usajili wa jengo, teknolojia za usindikaji wa mafuta ya kula, usajili wa biashara, usafi katika maeneo ya uzalishaji kama vile hotel, migahawa na maeneo mengine yanayohusiana na chakula na vipodozi.

“ Mnapaswa kufahamu kua serikali inahitaji ushiriki wenu katika vita ya umasikini ili kutekeleza hayo na hatimaye kufanikisha malengo ya kuifanya Tanzania kua nchi ya viwanda,” amesisitiza Makwaya

Kwa upande wake Meneja  wa Utafiti na Mafunzo wa Shirika la Viwango Tanzania (tbs), Mwl. Hamisi Mwanasala amewaagiza Wajasiriamali hao kuongeza thamani bidhaa zao ili waweze kuuza ndani na nje ya nchi.

Pia amewataka kua mabalozi kuwafikishia elimu wajasiriamali ambao hawakupata nafasi ya kuhudhuria mafunzo hayo.

Naye Afisa viwango kutoka katika Shirika hilo, Zena Issa amewaagiza  kuhakikisha kua bidhaa zao zinakua na brand au maelekezo muhimu yanapatikana kwenye kifungashio cha bidha hizo.

Halikadhalika amewakumbusha kua ufahamu wa watumiaji au walaji nchini umekua mkubwa kiasi kwamba huwa waangalifu wakati wa kununua bidhaa ili kupata bidhaa zilizothibitishwa ubora wake.

Aidha amewataka wajasiriamali kote nchini kuhakikisha bidhaa zao zinakidhi ubora kulingana na kiwango husika na zimethibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (tbs) ili  kuweza kutumia fursa ya soko la ndani na hata lile la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 

Katika mafunzo hayo Wajasiriamali wamejifunza mada ya viwango, matumizi na faida zake, utaratibu wa kupata leseni ya alama ya ubora wa bidhaa na usajili wa majengo, usafi wa maeneo ya kuuzia bidhaa za mafuta yakula, teknolojia za usindikaji bidhaa za mafuta ya kula, kanuni bora za uzalishaji na uhifadhi wa mafuta ya kula, utaratibu wa kufuata wakati wa urasimishaji wa biashara na huduma zitololewazo na ofisi maendeleo ya jamii.                                                                                                                                                                                                                                                                 

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Emmanuel Makwaya akiwa na wataalamu mbalimbali waliowasilisha mada kwa wazalishaji na wasindikaji wa  bidhaa ya mafuta ya kula katika semina ya Shirika la viwango Tanzania (tbs)  wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                     

Baadhi ya wazalishaji na wasindikaji wa  bidhaa ya mafuta ya kula wakiwa katika semina ya Shirika la viwango Tanzania (tbs) wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.