• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Singida katika ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wilayani Iramba, Suleiman Mwenda amesema kuwa falsafa, maono, maarifa na imani ya Rais Samia kujenga madarasa nchini imeleta tija ya wanafunzi kuanza masomo ya

Posted on: January 22nd, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Singida katika ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wilayani Iramba, Suleiman Mwenda amesema kuwa falsafa, maono, maarifa na imani ya Rais Samia kujenga madarasa nchini imeleta tija ya wanafunzi kuanza masomo yao bila ya kikwazo chochote.

Mwenda ameyasema hayo mwishoni mwa juma hili wakati akiwa na Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida wilayani Iramba katika shule ya sekondari Kinambeu mjini hapa.

Ziara hiyo inajiri ikiwa ni siku chache tangu wanafunzi wafungue shule kute nchini.

Alisema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za ujenzi wa madarasa ambayo yamekidhi mahitaji ya wanafunzi wote.

“Ndugu Mwenyekiti, tumshukuru Rais Samia kwa namna ya kipekee kwa fedha alizoleta, tumeweza kujenga madarasa 47 na kuweza kukidhi wanafunzi 1250.” Alisema

Aidha, aliongeza kuwa wanafunzi ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu ni wanafunzi 4022 ambapo ni ongezeko la takribani wanafunzi 800 ukilinganisha na idadi ya wanafunzi waliochaguliwa mwaka jana.

Alibainisha kuwa kama madarasa haya yasingejengwa kungekuwa na wanafunzi 1200 ambao wasingekuwa na madarasa ya kusomea lakini kwa ujenzi wa madarasa haya wanafunzi wote wanapata sehemu ya kusomea na ziada ya takribani wanafunzi 80.

“Kwa kweli tunamshukuru Rais Samia kwa sababu tumepata madarasa ambayo yanasamani zote ikiwemo meza, viti pamoja na ofisi za walimu.”

Halikadhalika, Mwenda amekipongeza Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa na ilani nzuri ambayo inaielekeza serikali kwamba wanafunzi wote wanaochaguliwa kujiunga na masomo kwa mwaka husika lazima wapate  sehemu za kusomea na kuwa na mazingira bora.

Akiongea katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa mkoa wa Singida, Alhaji Juma Kilimba alisema kuwa ujenzi wa madarasa hayo umeboresha manzari ya shule na mji kwa ujumla.

“Hii ndio manzari ya kiomboi, leo unapoingia wilayani unakuta shule imependeza namna hii, hakika hili ni jambo la faraja sana.” Alipongeza

Aidha amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora kuona namna ya kuhakikisha shule ya Sekondari Kinambeu inapata bwalo la wanafunzi.

Awali akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Kamati hiyo, Mkuu wa shule ya Sekondari Kinambeu, Godfrey Yohana amemuhakikishia Mwenyekiti huyo, kuwa watayatumia madarasa hayo kwa lengo la kuhakikisha wanafunzi wanafaulu vizuri.

Kw upande wake mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo ambaye yupo kidato cha kwanza, Warda Mohammed amemshukuru Rais Samia kwa kusaidia kuwaletea fedha za ujenzi wa madarasa na madawati ambayo itakuwa rahisi kwao kusoma, kuandika na kuokoa muda.

Aidha, ameongeza kuwa madawati hayo yamepunguza mzigo uliokuwepo wa kuwataka wazazi kupeleka madawati shuleni.

Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Singida ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilitembelea mradi wa maji kata ya Maluga, mradi wa shule shikizi kata ya Ulemo na Mradi wa madarasa kata ya Old Kiomboi wilayani Iramba.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.