• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Kamati ya Fedha Mipango na Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imefanya ziara kukagua ujenzi wa stendi mpya ya mabasi ya Misigiri inayojengwa kijiji cha Misigiri kata ya Ulemo

Posted on: March 5th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kuongeza kasi ya ujenzi wa stendi mpya ya mabasi ya Misigiri inayojengwa kijiji cha Misigiri kata ya Ulemo.

Tyosela ametoa agizo hilo leo Alhamisi Machi 5, 2020 wakati walipofanya ziara katika eneo hilo akiwa na Kamati ya Fedha Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo.

Katika ziara hiyo ameagiza kasi ya ujenzi iongezeke huku akiitaka kamati ndogo ya Ujenzi kuhakikisha barabara ya kuchepuka wakati wa kuingia na kutoka katika stendi hiyo inakamila mara moja.

“Ninaagiza kasi ya ujenzi iongezeke na kuhakikisha barabara za mchepuko zinakamila kwa wakati,”amesisitiza Tyosela

Akisoma taarifa ya ujenzi wa stendi hiyo, Mchumi wa Halmashuri, Mapenzi Lenjima amesema takribani Tshs11.81 milioni zimekisiwa kukamilisha ujenzi huo.

Amefafanua kuwa mpaka sasa ujenzi umefika hatua ya  lenta ambapo Tshs5.9 milioni zimetumika kujenga choo chenye matundu matatu ya wanaume na matundu matano ya wanawake.

Pia amewakumbusha waliopewa vibanda kulipa Tshs 50,000 ili kukamilisha ujenzi kwa wakati huku akiwatahadharisha wale watakaoshindwa kulipia kuwa vibanda watapewa waliokuwa tayari kulipia.

Aidha amesema wanatarajia kujenga jengo la kupumzikia abiria na kibada cha polisi.

Kamati ya Fedha Mipango na Utawala ya Halmashuri hiyo imeendelea na ziara mpaka kijiji  cha Nselembwe kata ya  Shelui eneo  ambalo  litajengwa kituo cha Afya.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Hussein Sepoko ameishukuru serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuleta Tshs400 milioni za ujenzi wa kituo hicho.

Sepoko amesema kuwa majengo matano yanatarajiwa kujengwa ambayo ni jengo la mama na mtoto, jengo la upasuaji (theater), nyumba ya mtumishi, jengo la kufulia (laundry), jengo la kuhifadhia maiti(mortuary) na jengo la maabara (laboratory).

Katika ziara hiyo wajumbe wa kamati hiyo walipata fursa yakutoa mapendekezo mbalimbali.

 

Diwani wa kata ya Ntwike, Albert Makwala aliishauri kamati ya ujezi wa kituo hicho kuchukua tahadhari ya mkondo wamaji unaopita katika eneo hilo huku akiitaka kamati hiyo kutegemea ushauri wa kitaalamu.

Naye Diwani wa kata ya Kyengege Innocent Msengi aliitaka kamati hiyo kuongeza kasi ya ujenzi wa kituo cha Afya nakuhakikisha kutokuwa na madoa doa.

Halikadhalika amewataka waungane ili wafanye mabadiliko ya haraka kwa kuwa fedha wanazo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Samwel Shillah ameuagiza uwongozi wa kata ya Shelui kupanda miti katika mipaka ya eneo hilo na kuhakikisha  barabara zinatengenezwa vizuri na kuacha lango kuu la kuingilia kituoni hapo linakua moja.

Ziara ya Kamati ya Fedha Mipango na Utawala imetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa stendi mpya ya mabasi ya Misigiri inayojengwa kijiji cha Misigiri kata ya Ulemo, mradi wa kituo cha Afya utakojengwa kijiji cha Nselembwe kata ya Shelui na mradi wa nyumba ya Walimu, bweni la wanafunzi na bwalo la wanafunzi vinavyojengwa katika shule ya sekondari Shelui.                                              

Kamati ya Fedha Mipango na Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ikikagua eneo la kijiji cha Nselembwe kata ya Shelui ambalo litajengwa kituo cha Afya kwa  fedha zilizoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwaonesha baadhi ya wakuu wa Idara wa Halmasghauri hiyo eneo la kijiji cha Nselembwe kata ya Shelui ambalo litajengwa kituo cha Afya kwa  fedha zilizoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Picha na Hemedi Munga                                                                                         

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwa na baadhi ya wakuu wa Idara wakati wa kukagua eneo la kijiji cha Nselembwe kata ya Shelui ambalo litajengwa kituo cha Afya kwa  fedha zilizoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Picha na Hemedi Munga                                                                                                 

Mwandishi wa vikao vya Halmashauri, Ndugu Neema akiwa na Diwani wa kata ya shelui katikati, Kinota Hamisi na kulia mwa Diwani huyo ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Samwel Shillah. Picha na Hemedi Munga

Mradi wa nyumba ya walimu unaojengwa shule ya sekondari Shelui. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                             

Mradi wa bweni unaojengwa shule ya sekondari Shelui. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                 

Afisa Elimu sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Godfrey Mwanjala akionesha jambo wakati wa ukaguzi wa  Kamati ya Fedha Mipango na Utawala shule ya sekondari ya Shelui. Picha na Hemedi Munga

Mradi wa bwalo unaojengwa shule ya sekondari Shelui. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.