• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala yatembelea na kukagua miradi ya maendeleo yenye Tsh 1.6 bilioni Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Posted on: January 21st, 2021

Hemedi Munga. Irambadc

Irambadc@singida.go.tz

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, John Magufuli ambayo imeendelea kuleta fedha za miradi ya maendeleo Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Msengi ameyasema hayo leo Alhamisi Januari 21, 2021 wakati akiwa na kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wa Halmashauri hiyo, Tumaini Sekondari kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa wilayani hapo.

Amewaagiza wataalamu na kamati mbalimbali za ujenzi wa miradi hiyo kuingiza nguvu za   wananchi katika taarifa zao ili kuonesha namna ambavyo wanaiunga serikali mkono katika kuwaletea Wananchi maendeleo.

Katika hatua nyingine, Msengi amewataka Walimu  Wakuu na Wakuu wa shule zote Wilayani humo kuhakikisha wanafunzi wote wanaostahili  kwenda shule wemefika na kuanza masomo.

Akihoji mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala kuhusu kukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati, Peter John amesema muda uliobakia ni mchache je miradi hii itakamilika kwa wakati uliopangwa.

Akijibu hoja ya mjumbe wa kamati ya fedha, Mipango na Utawala mmoja wa wataalamu wanaosimamia miradi ya  shule ya Msingi Bomani kunakojengwa madarasa mawili, Hassan Mwanga amesema kuwa miradi hiyo itakamilika kwa wakati kwa kuwa fedha na malighafi vya kumalizia vipo na kwa kuzingatia mikataba ya mafundi inayowataka wamalize kabla ya januari 31, mwaka huu.

Kwa upande wake mjumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala, Jenifer Miano ameziomba kamati za ujenzi wa miradi hiyo kuongeza kasi, usimamizi wa dhati na wenye ufanisi  ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kiwango stahiki.

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo, imetembelea baadhi ya miradi yenye takribani Tsh 1.6 bilioni.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa madarasa mawili shule ya msingi Kiomboi Bomani, ujenzi wa hostel shule ya sekondari Lulumba, ukarabati na ujenzi wa miundombinu mbalimbali shule ya sekondari Tumaini, ujenzi wa kituo cha afya Shelui, ujenzi wa stendi ya Misigiri na ujenzi wa madarasa matatu shule ya msingi Kyengege.

Mwisho

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ikiwa mbele ya moja ya jengo la Kituo cha Afya Shelui Wilayani Iramba ,Mkoa wa Singida wakisikiliza taarifa ya ujenzi wa kituo hicho baada ya kutembelea na kukagua ujenzi huo. Picha na Hemedi Munga

Hatua ya ujenzi wa Hosteli shule ya sekondari Lulumba ilipofikia siku chache ilipotembelewa na kukaguliwa na Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala. Picha na Daudi Mujungu

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wakiwa katika viwanja vya Lulumba Sekondari wakisikiliza taarifa ya ujenzi wa Hosteli baada ya kutembelea na kukagua ujenzi huo. Picha na Daudi Mujungu


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.