• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: May 6th, 2025

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO


Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa ajili ya robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025, kwa lengo la kufuatilia utekelezaji na thamani ya fedha kwenye miradi hiyo.


Ziara hiyo ilifanyika, 24 Aprili 2025 ambapo kamati ilitembelea miradi kadhaa inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ya wilaya, ikiwemo: Mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Yombo wenye thamani ya shilingi milioni 318.8, Ujenzi wa Shule ya Msingi Nkokilangi (Mil. 250), Ujenzi wa Zahanati ya Mseko (Mil. 250), Ujenzi wa Shule mpya ya Amali katika Kijiji cha Kitukutu (Bil. 1.6), Kituo cha Kilimo cha Mampanta (Mil. 109.72).


Akizungumza baada ya kukamilika kwa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi, alieleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Msingi Yombo, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya ujenzi kwenye miradi mingine hususan Shule mpya ya Amali Kitukutu pamoja na Zahanati ya Mseko.


Aidha, Msengi alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo. Pia alitoa Pongezi kwa Mbunge wa Iramba Magharibi na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba pamoja na viongozi wengine kwa juhudi zao za kuwahudumia wananchi wa Iramba.


“Kwanza namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha za miradi hii. Pia nampongeza Mbunge wa Iramba Magharibi na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kuwahudumia Wananchi wa Iramba, Pongezi pia kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kwa usimamizi mzuri. Rai yangu ni kwamba usimamizi uendelee ili miradi ikamilike kwa wakati na kwa ubora unaostahili,” alisema Mheshimiwa Msengi.



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.