• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Kanisa la EAGT latumia 13.5milioni kuchangia vifaa vya kuchukua tahadhari ya kujikinga na corona na kunufaisha familia 75 kwa mikopo isiyokua na fidia wala marejesho Wilayani Iramba.

Posted on: May 25th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amegawa ndoo za maji ya kutiririka 282 na sabuni katoni 12 kwa Wazazi wa Watoto wanaohudumiwa na Kanisa la EAGT Kiomboi wakishirikiana na Compassion International Tanzania.

Mwageni amegawa vifaa hivyo leo May 24, 2020 baada ya ibada fupi iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la EAGT mjini Kiomboi.

Amewaagiza wazazi wote waliopatiwa vifaa hivyo kuvitumia ili kuendelea kuchukua tahadhari ya  maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona na sio kwenda kuviweka kama mapambo katika majumba yao.

Pia, amewaomba kuacha tabia ya kuwatumia wanafunzi katika shughuli za uchumi kama vile kuwapeleka sokoni, madukani na minadani ili kuwaepusha na maambukizi ya corona.

“Niwaombe wazazi wenzangu kuwaandaa wanafunzi wa kidato cha 6 na vyuo kwa kuwanunulia barakoa, sanitaiza na pesa kwa ajili ya kununua machungwa, malimao na Tangawizi,” ameomba Mwageni na kuongeza

 

“Kwa upande wa kidato cha pili na cha nne Halmashauri imeandaa Makala mbalimbali ambazo zitawafikia wanafunzi hao kupitia watendaji wa vitongoji vyao.”

Halikadhalika, Mwageni amewaagiza Wazazi hao kuwahimiza wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha kwanza, tatu, na cha tano kutumia muda wao kutazama vipindi vya masomo mbalimbali vinavyorushwa na Chanel Ten, Azam TV, TBC na ZBC.

“Katika kipindi hichi cha kusubiria maelekezo ya Serikali ,wanafunzi wanawajibu wa kubadilisha namna ya kujifunza kutoka darasani hadi barazani kwa kutazama vipindi vya masomo mbalimbali kupitia Chanel Ten, Azam TV, TBC na  ZBC,” amesema Mwageni

Katika hatua nyingine, Mwageni amemshukuru Mchungaji wa Kanisa la EAGT, Robert Kijanga kwa kuwalea watoto hao, kwani kitendo hicho kimeifanya Wilaya ya Iramba kutokua na Watoto wa mitaani na omba omba.

Naye Mchungaji wa Kanisa la EAGT kiomboi, Robert Kijanga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna alivyopambana na janga la corona bila kufunga Makanisa, Misikiti na shughuli za kiuchumi.

“Rais huyu ameishangaza Dunia nzima kwa namna alivyopambana na janga la corona kwa kuweka rehani maisha yake kwa Mungu kuliko kujifungia ndani bila Mungu, ameruhusu Makanisa na Misikiti waumini waendelee kumuomba Mungu, na ndio maana tunakabiliana na corona vyema na kwa sababu hiyo leo tumeshinda na leo ni siku ya pekee na ya kumshukuru Mungu kwa kuwa tumeshinda,” amesema Kijanga na kuongeza

 

“Mhe, Rais ameliokoa Taifa kuto kuingia katika hali mbaya kwa kuwa tumeendelea kuchapa kazi, leo hii Mataifa Makubwa yalioendelea yalijifungia na leo yanajifungua na kutukuta pale pale tulipokuwepo.”

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo cha Huduma ya Mtoto wa Kanisa la EAGT, Gerald Adoltia alipokua akitoa taarifa fupi mbele ya  Mkurugenzi Mtendaji, Linno Mwageni amesema kuwa wamekuwa na utaratibu wakutoa elimu ya kiroho, kimwili, kiuchumi na kijamii kila siku ya jumamosi  kwa watoto 282 tangu Novemba 14, 2014.

Akibainisha malengo ya kuwafundisha watoto hao kujikomboa toka katika umasikini, amesema kuwa wamekua wakiwapatia watoto hao daftari, viatu, nguo za shule, kalamu, mabegi na kugharamia matibabu pindi wanapougua.

Pia, kutoa mitaji kwa familia takriban 75 ambapo jumla ya Tshs 10milioni zimetumika kuzinufaisha familia kuboresha maisha yao kiuchumi bila kudai fidia wala marejesho yoyote kutoka kwao.

Familia hizo zimekuwa zikipatiwa mafunzo ya Afya, ujasiriamali wa nadharia na vitendo, ufugaji, malezi ya familia na ndoa, kilimo, ulinzi wa mtoto, elimu ya fedha na mipango pamoja nakujengewa uwezo wa kupambana na magonjwa ya ukimwi na malaria.

Naye mmoja wa Wazazi waliogawiwa vifaa hivyo, Martha Edson amewashukuru viongozi wa Kanisa la EAGT kwa kuwapatia ndoo na sabuni na kuwaombea Mungu awabariki.

 MWISHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwaasa wazazi kuwanunulia wanafunzi barakoa na kuhakikisha wanawahimiza Wanafunzi kufuatilia vipindi vya masomo kwenye Chaneli Ten, TBC, ZBC na Azam TV. Picha na Hemedi Munga

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Kiomboi akiombea Wilaya ya Iramba na Taifa kuepukana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Mdhibiti wa maambukizi ya corona wa Hospitali ya Wilaya ya Iramba, Yona Mwasanga akiwaonesha Waumini wa Kanisa la EAGT namna ya kunawa na kusugua viganja vya mikono kwa vitendo ili waendelee kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwa na Mchungaji Robert Kijanga pamoja na wataalam wengine punde baada ya kugawa ndoo na sabuni. Picha na Hemedi Munga

Ndoo 282 na katoni 12 za sabuni zilizotolewa na Kanisa la EAGT Kiomboi kwa Wazazi wa Watoto wanaohudumiwa na Kanisa hilo kwa kushirikiana na Compassion International Tanzania. Picha na Hemedi Munga

Ndoo 282 na katoni 12 za sabuni zilizotolewa na Kanisa la EAGT Kiomboi kwa Wazazi wa Watoto wanaohudumiwa na Kanisa hilo kwa kushirikiana na Compassion International Tanzania. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • WAHI NAFASI YA AJIRA August 19, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • TANGAZO LA KULIPA KODI YA ARDHI. February 26, 2018
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WAPANDA MITI 3500 KATA YA MGONGO

    March 09, 2023
  • PIKIPIKI SITA ZAKABIDHIWA KWA WATENDAJI WA KATA.

    March 09, 2023
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI IRAMBA

    March 08, 2023
  • ZIARA YA WAH MADIWANI WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA, MIPANGO NA UTAWALA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO TAREHE 23 JANUARI, 2023

    January 23, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.