• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dtk. Angelina Lutambi akiwaasa Wakuu wa Shule matumizi ya mfumo wa TANePS. Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 16th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi amefungua  mafunzo ya  siku moja ya mfumo wa manunuzi ya umma kwa njia ya mtandao (TANePS) kwa Wakuu wa Shule za Sekondari na Walimu wakuu wa shule za Msingi.

Mafunzo hayo yamefunguliwa leo Alhamisi Januari 16, 2020 katika Ukumbi  mkubwa wa  Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mjini  Kiomboi.

Dkt, Lutambi amewaagiza viongozi hao kutimiza wajibu wao na kuhakikisha kuwa kila kitu katika taasisi zao kinafuata sheria, taratibu na kanuni na miongozo kama ilivyoagizwa na Serikali.

‘’Serikali ya sasa imeamua kupeleka pesa katika mamlaka zenu  kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi na hivyo sheria haitambui endapo kiongozi au mtumishi aliyoko chini ya kiongozi huyo atakapoharibu,

mmekabidhiwa dhamana ya kuhakikisha pesa zinazoletwa na serikali zinatumika katika malengo stahiki.”

“ Nyinyi ni maafisa masuuli na mnao wajibu kuhakikisha taratibu zote za manunuzi zinazingatiwa,”  amesisitiza Dkt, Lutambi

Kufuata taratibu na kanuni za manunuzi zitapunguza uwepo wa hoja za ukaguzi zitokanazo na manunuzi wilayani hapa.

Aidha Dkt, Lutambi amewataka viongozi hao kutumia mfumo wa manunuzi ya umma kwa njia ya mtandao (TANePS) ambapo mwisho wa kufanya manunuzi nje ya mfumo ilikuwa Desemba 31mwaka jana.

Hatua hiyo itasaidia serikali kufahamu manunuzi yanayofanyika katika kila mwezi na hivyo kuiwezesha kupanga mipango yake.

Hata hivyo amewatahadharisha viongozi hao watakaofanya manunuzi nje ya mfumo wa manunuzi ya umma kwa njia ya mtandao  na kukwamisha shughuli mbalimbali katika taasisi husika hawatoeleweka.

Amefafanua kuwa mfumo huo unaleta uwazi unaomuwezesha msambazaji yoyote wa bidhaa aliyesajiliwa kuwa anaweza kusambaza bidhaa hata kama atakuwa mkoa mwingine.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amewakumbusha viongozi hao kuwa pamoja na kuwa swala la manunuzi sio fani walizosomea bali wanapaswa kufahamu kuwa barua walizopewa na mwajiri wao zinawataka kutekeleza na majukumu mengine watakayopangiwa.

Awali akielezea mzunguko wa manunuzi Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Afisa manunuzi na Ugavi , Ibrahimu Nkumbi amesema manunuzi ni hatua kwa hatua zinazojumuisha shughuli muhimu zinazohitajika katika kukamilisha manunuzi.

Nkumbi amezitaja hatua hizo kuwa ni utambuzi wa mahitaji ya manunuzi, kupanga mpango wa manunuzi, mchakato wa manunuzi, utoaji tuzo ya mkataba, utekelezaji usimamizi wa mkataba na tathimini ya mkataba.

Akichangia mada mkuu wa shule ya Tumaini Sekondari, Honoratha Mbiaji amemuhakikishia Katibu Tawala huyo kuwa mafunzo hayo wanayoyapata watayafanyia kazi kwa ukamilifu.

Naye  Mkuu wa Shule ya Lulumba Sekondari, Jeremia Kitiku ameuomba uongozi kufikisha mafunzo hayo kwa sekta mbalimbali ikiwemo  afya.                                                                                                                                                             

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Afisa manunuzi na Ugavi , Ibrahimu Nkumbi akiwafafanuliya Wakuu wa Shule mzunguko wa manunuzi katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Iramba. Picha na Hemedi Munga                                  

Wakuu wa Shule (TAHOSA) na Walimu wakuu (TAPSHA) wakifuatilia mafuzo kwa umakini  katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.