• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi emegawa kompyuta kwa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba zilizoingia kumi bora kimkoa Singida matokeyo ya mwaka 2019.

Posted on: June 5th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi emegawa kompyuta kwa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba zilizoingia kumi bora kimkoa Singida matokeyo ya mwaka 2019.

Lutambi amegawa kompyuta hizo (desktop) mwishoni mwa juma hili wakati alipokua akiongea na Baraza maalum la Madiwani kujibu maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mjini Kiomboi.

Ametumia nafasi hiyo kumshukuru aliyetoa kompyuta hizo hasa katika nyakati hizi ambazo kila kitu kinaendeshwa kielektroniki.

“Kwa sasa ni zama za kielektroniki, nilazima tushukuru kwa kupata kompyuta hizi kwa sababu walimu watatekeleza majukumu ya kielimu, Serikali na kuandaa mitihani na majaribio mbalimbali ya wanafunzi ili waweze kufanya vizuri,” amesema Lutambi nakuongeza

“Kompyuta hizo zitawasaidia walimu kupata maarifa mapya na marejeo mbalimbali ili kujipatia maarifa mapya kulingana na masomo yao wanayofundisha, hivyo kuwa na weledi na kupata mawazo mapya yanayoendana na wakati huu tulionao.”

Hatua hiyo itawasaidia Walimu kuondokana na matumizi ya notsi za zamani walizozitumia wao wakiwa shuleni, huku akiwasihi kuzitumia vizuri.

“Niwasihi ndugu zangu Wakuu wa Shule kuwa kompyuta hizi sio binafsi, zimetolewa kwa shule na nyinyi mmekuja zipokea kwa niaba ya shule zenu, kwa hiyo niwaombe kwa kushirikiana na walimu wenzenu mkazitumie vizuri,” amesisitiza Lutambi

Kompyuta hizo zilizogawiwa kwa shule hizo ni ahadi ambayo aliahidi Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba alipokua akizungumza katika Baraza la Madiwani Juni 02 mwaka huu.

“Ninawapatia kompyuta mpya za kisasa za shule nne zilizoingia kumi bora kimkoa Singida ili kuweza kusaidia taratibu hizi za kisasa za uandaaji wa masomo ya wanafunzi,” alisema Waziri Nchemba

Lengo likiwa ni kuwachochea Walimu kwa kazi nzuri wanazo zifanya chini ya usimamizi mzuri wa Mkuu wa Wilaya yetu, Emmanuel Luhahula.

Akishuhudia ugawaji wa kompyuta hizo kwa shule zilizokua na ufaulu mzuri matokeo ya mwaka jana, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo, Godfrey Mwanjala amesema kuwa kompyuta hizo zitasaidia maandalizi mbalimbali ya majukumu ya walimu kwa wanafunzi wao.

Mwanjala amezitaja shule hizo kuwa ni Kyengege Sekondari, Kisana Sekondari, Mgongo Sekondari na Kidaru ambazo zimeingia kumi bora kimkoa Singida.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Shule waliopatiwa kompyuta hizo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mgongo, Lameck Ayieko ameshukuru kwa kupatiwa msaada huo wa kompyuta na kuahidi kuwa watazitumia kwa manufaa ya shule zao na kuzituza vizuri.

MWISHO

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mgongo, Lameck Ayieko akipokea kompyuta toka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Picha na Hemedi Munga

Afisa Elimu kata ya Kyengege, Daudi Kachilu akipokea kompyuta kwa niaba ya Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kyengege zilizotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).


Baadhi ya Kompyuta zilizotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.