• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi emegawa kompyuta kwa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba zilizoingia kumi bora kimkoa Singida matokeyo ya mwaka 2019.

Posted on: June 5th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi emegawa kompyuta kwa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba zilizoingia kumi bora kimkoa Singida matokeyo ya mwaka 2019.

Lutambi amegawa kompyuta hizo (desktop) mwishoni mwa juma hili wakati alipokua akiongea na Baraza maalum la Madiwani kujibu maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mjini Kiomboi.

Ametumia nafasi hiyo kumshukuru aliyetoa kompyuta hizo hasa katika nyakati hizi ambazo kila kitu kinaendeshwa kielektroniki.

“Kwa sasa ni zama za kielektroniki, nilazima tushukuru kwa kupata kompyuta hizi kwa sababu walimu watatekeleza majukumu ya kielimu, Serikali na kuandaa mitihani na majaribio mbalimbali ya wanafunzi ili waweze kufanya vizuri,” amesema Lutambi nakuongeza

“Kompyuta hizo zitawasaidia walimu kupata maarifa mapya na marejeo mbalimbali ili kujipatia maarifa mapya kulingana na masomo yao wanayofundisha, hivyo kuwa na weledi na kupata mawazo mapya yanayoendana na wakati huu tulionao.”

Hatua hiyo itawasaidia Walimu kuondokana na matumizi ya notsi za zamani walizozitumia wao wakiwa shuleni, huku akiwasihi kuzitumia vizuri.

“Niwasihi ndugu zangu Wakuu wa Shule kuwa kompyuta hizi sio binafsi, zimetolewa kwa shule na nyinyi mmekuja zipokea kwa niaba ya shule zenu, kwa hiyo niwaombe kwa kushirikiana na walimu wenzenu mkazitumie vizuri,” amesisitiza Lutambi

Kompyuta hizo zilizogawiwa kwa shule hizo ni ahadi ambayo aliahidi Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba alipokua akizungumza katika Baraza la Madiwani Juni 02 mwaka huu.

“Ninawapatia kompyuta mpya za kisasa za shule nne zilizoingia kumi bora kimkoa Singida ili kuweza kusaidia taratibu hizi za kisasa za uandaaji wa masomo ya wanafunzi,” alisema Waziri Nchemba

Lengo likiwa ni kuwachochea Walimu kwa kazi nzuri wanazo zifanya chini ya usimamizi mzuri wa Mkuu wa Wilaya yetu, Emmanuel Luhahula.

Akishuhudia ugawaji wa kompyuta hizo kwa shule zilizokua na ufaulu mzuri matokeo ya mwaka jana, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo, Godfrey Mwanjala amesema kuwa kompyuta hizo zitasaidia maandalizi mbalimbali ya majukumu ya walimu kwa wanafunzi wao.

Mwanjala amezitaja shule hizo kuwa ni Kyengege Sekondari, Kisana Sekondari, Mgongo Sekondari na Kidaru ambazo zimeingia kumi bora kimkoa Singida.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Shule waliopatiwa kompyuta hizo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mgongo, Lameck Ayieko ameshukuru kwa kupatiwa msaada huo wa kompyuta na kuahidi kuwa watazitumia kwa manufaa ya shule zao na kuzituza vizuri.

MWISHO

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mgongo, Lameck Ayieko akipokea kompyuta toka kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Picha na Hemedi Munga

Afisa Elimu kata ya Kyengege, Daudi Kachilu akipokea kompyuta kwa niaba ya Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kyengege zilizotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).


Baadhi ya Kompyuta zilizotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba zilizogawiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa kikao maalum cha kushughulikia maagizo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).


Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.