• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

KIKAO CHA KAMATI YA LISHE NGAZI YA HALMASHAURI KWA KIPINDI CHA ROBO YA TATU YA MWEZI JANUARI HADI MACHI 2024 CHAFANYIKA

Posted on: May 19th, 2025

KIKAO CHA KAMATI YA LISHE NGAZI YA HALMASHAURI KWA KIPINDI CHA ROBO YA TATU YA MWEZI JANUARI HADI MACHI 2024 CHAFANYIKA


Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imefanya kikao cha Kamati ya Lishe ili kujadili taarifa ya utekekelezaji wa Afua za Lishe kwa kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambacho kimefanyika Mei 19, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.


Kikao hicho kimeongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi wa Mazingira na udhibiti Taka Ndug. Jeremia Kahurananga kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri na kimeketi kujadili taarifa hiyo kwa Kitengo cha Huduma za Lishe, Idara ya Elimu ya awali na Msingi, Idara ya Elimu Sekondari, Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Divisheni ya Maendeleo ya Jamii.


Akizungumza katika kiako hicho Kahurananga ametoa rai kwa wajumbe wa kikao kwenda kuyatekeleza yote yaliyojadiliwa katika kikao hicho ikiwa ni pamoja na kuhakikisha afua za Lishe zinatekelezwa ipasavyo kama zilivyokusudiwa.


“Twende tukayatekeleze tuliyo yajadili kwa umakini ili kufikia malengo tuliyokusudia katika kutekeleza afua za Lishe .” Amesema Kahurananga.


Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa robo ya Tatu Afisa Lishe wa Halmashauri Mary Assey amesema kwa kipindi hicho Jumla ya akina mama/walezi 22,301 (100%) wenye Watoto wenye umri wa miezi 0-23 wamepewa elimu juu ya unyonyeshaji wa watoto wachanga na ulishaji wa Watoto wadogo kupitia watoa huduma ngazi ya vituo vya kutolea huduma za afya, na 7,976 (100%) wamepewa elimu hiyo kupitia watoa huduma ngazi ya jamii.


Pia, jumla ya akina mama wajawazito 13,302 (97.92%) kati ya wajawazito 13,482 waliohudhuriwa kliniki ya uzazi na mtoto, walipewa vidonge vya kuongeza damu, vidonge vya madini chuma na asidi ya foliki vya kutosha hadi hudhurio linalofuata.


Kwa upande wa utoaji chakula shule za Msingi na Sekondari, jumla ya shule 138 (98.6%) kati ya shule 140 zimefanikiwa kutoa chakula kwa wanafunzi angalau mlo mmoja kwa siku. Na jumla ya wanafunzi 69084 (99.8%) kati ya 78480 wanapata chakula muda wawapo shuleni.


Tangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI KUJADILI NA KUPOKEA TAARIFA YA CAG MWAKA WA FEDHA 2023/2024 TAREHE 18, JUNI 2025 June 16, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI

    July 08, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 2025

    July 07, 2025
  • TRA IRAMBA YAVUKA MALENGO YA UKUSANYAJI KODI KWA ASILIMIA 130, YAWASHUKURU WALIPAKODI

    July 01, 2025
  • DC MWENDA AKABIDHI SPIKA KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII IRAMBA

    July 01, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.