• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

KITUO CHA AFYA TYEGELO CHAZINDULIWA RASMI TAYARI KWA AJILI YA KUANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA NA KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA AFYA KWA WANANCHI KAMA SIYO KUZIONDOA KABIS

Posted on: September 18th, 2023

KITUO CHA AFYA TYEGELO CHAZINDULIWA RASMI TAYARI KWA AJILI YA KUANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA NA KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA AFYA KWA WANANCHI KAMA SIYO KUZIONDOA KABISA

Wananchi wa Kata ya Kidaru,Tarafa ya Kisiriri Wilaya ya Iramba Mkoani Singida,Wametakiwa kumwonyesha  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani,Uungwana wa kumpigia kura za Ndiyo kwa kazi kubwa anazozifanya za kuleta miradi mingi ya Maendeleo kama vile Kituo Cha Afya Tyegelo kilichopo Kata ya Kidaru ambacho ilikuwa ni ndoto kwa Wananchi wa Kata hiyo.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda ambaye alikuwa mgeni Rasmi Katika Uzinduzi wa Kituo Cha Afya Tyegelo kilichopo Kata ya Kidaru,Tarafa ya Kisiriri Wilayani Iramba uzinduzi uliofanyika  Septemba 16,Mwaka huu katika Kijiji Cha Tyegelo, Tayari kwa kuwahudumia Wananchi wa eneo Hilo la bonde la ufa .


Aidha DC Mwenda amesema takribani Miaka miwili na nusu ya Uongozi wa Rais Samia ametoa miradi mingi sana katika Wilaya ya Iramba pamoja na nchi nzima,Lakini katika Kata ya Kidaru Mama Samia ameleta Miradi katika Shule ya Msingi Mwamapuli,ambapo takribani Milioni 250 zimepelekwa kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba 4 na Madarasa Mawili mapya kwa ajili ya wanafunzi pamoja na Matundu 24 ya Vyoo vya wanafunzi  katika Shule hiyo.


Amesema katika Shule ya Sekondari Kidaru serikali imeleta Jumla ya Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya Ujenzi wa Madarasa Sita,ikiwemo ujenzi wa Hosteli kwa ajili ya watoto wa kike ambao uligharimu Shilingi Milioni 70  kwa ajili ya ukamilishwaji wa jengo hilo.Hata hivyo ameongeza kuwa siyo hivyo tu na Shule ya Msingi Kidaru nako serikali ikatoa Shilingi Milioni 11 kwa ajili ya umaliziaji  wa Darasa moja,Ujenzi wake Tayari umekamilika.

Kiongozi huyo akiwaleleza Wananchi kazi zilizofanywa na serikali ya awamu ya Sita,inayoongozwa na Mama Samia,amesema si hivyo tu hata barabara ambayo inatoka Kidaru Tyegelo Luono hadi Makao makuu ya Wilaya Kiomboi lakini Fedha zililetwa na serikali ambazo ni Bilioni 3 na Milioni 500 ambazo sasa zinajenga karavati katika barabara ya Tyegelo hadi Ndurumo na kuelekea Mto Sibiti na inatarajiwa kijengwa kwa Kiwango cha lami

DC Mwenda ameeleza kuwa hivi "Hapa tulipo Leo tunazindua Kituo Cha Afya Tyegelo  Kata hii ya Kidaru ,Kituo ambacho ilikuwa ni ndoto lakini mama kwa huruma zake kwa Wananchi wa Kata ya Kidaru akatoa Tsh. Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo hiki ambapo Leo Tunakizindua" amesema DC Mwenda.

Licha ya hayo amesema pia Jumla ya Tsh. Milioni 800,Zimenunua vifaa tiba kwa lengo la kutoa  huduma Bora na za kisasa .


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.