• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Lulumba Sekondari ya shika nafasi ya Sita kati ya Shule 737 Kitaifa kwa somo la jografia na kuwa ya kwanza Mkoa wa Singida kwa masomo yote.

Posted on: August 21st, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Shule ya Sekondari Lulumba,Jeremia Kitiku amesema kuwa Lulumba Sekondari  imekuwa ya kwanza Kimkoa kati ya shule 12 za Mkoa wa Singida na ya 23 Kitaifa kati ya shule 586 katika matokeo ya Kidato cha Sita yaliotangazwa na Katibu wa Baraza la Mitihani Tanzania, Dkt, charles Msonde.

Kitiku ameyasema hayo leo ijumaa agosti 21, 2020 wakati akiongea na mwandishi wetu katika viwanja vya Shule hiyo mjini Kiomboi.

“Nijambo la Kumshukuru Mungu na kuwapongeza Wanafunzi kwa matokeo mazuri waliyoyapata yanafurahisha sana,” amesema Kitiku na kufafanua kuwa

“Wanafunzi waliofanya Mtihani walikuwa 151 ambapo 85 wamepata daraja la kwanza, 53 daraja la pili, 13 daraja la tatu na hakuna aliyepata 0,”

Kufuatia hatua hiyo amewapongeza Walimu wa Shule kiyo ambao wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi unaongezeka ili kuifikisha Shule hiyo ndani ya kumi bora kitaifa.

 

“Ndugu walimu wenzangu nawapongeza sana kwa kazi na juhudi kubwa mnazozifanya kuhakikisha wanafunzi wanakuwa vizuri kabla ya mtihani wa Taifa, hivyo leo tunasherehekea matokeo mazuri” amepongeza na kuongeza kuwa

“Kwa masomo ya jografia, fizikia, kemia, baiolojia, hesabu, GS na bam yanayofundishwa hapa tumeshika nafasi ya kwanza kimkoa na kushika nafasi nzuri kitaifa”

Akieleza siri ya mafanikio hayo Mkuu huyo wa Shule, amesema kuwa huwa wanatekeleza  mkakati wa kumaliza silabasi mapema kisha wanafanya marudio na kuwatahini Wanafunzi Mitihani ya mara kwa mara.

Amebainisha kuwa wanao ushirikiano wa kimasomo na mitihani na shule ambazo zinafanya vizuri Kitaifa ikiwemo Tabora boys.

Akizungumzia ari na kasi ya walimu wanaojitoa kutekeleza mikakati hiyo amesema kuwa ni zawadi mbalimbali zinazotolewa na Shule ikiwemo Tsh 20,000 pindi Mwalimu anapofanikisha Mwanafunzi kupata A, na Tsh 10,000 mwanafunzi anapopata B, Hivyo kuongeza ari ya kujituma katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

“Tunahakikisha kuwa Walimu wanapata chai na kitafunwa asubuhi chakula cha mchana kwa Walimu wote kwa gharama za Shule hivyo kuwafanya walimu kufundisha kwa ushindani,” amebainisha

 

Akibainisha mbinu na njia anazozitumia Mwalimu wa Jografia aliyefanikisha somo hilo kushika nafasi ya sita kitaifa, Daud Noa amesema kuwa ni mara ya kwanza kwa somo hilo kufundishwa katika shule hiyo kwa sababu mchepuo huo haukuwepo.


“Ni mara ya kwanza kwa mchepuo unaohusisha somo la jografia katika shule yetu, hivyo tumefanikiwa kushika nafasi ya sita kati ya Shule 737 kitaifa huku kimkoa na kiwilaya kushika nafasi ya kwanza,” amesema Noa

Mikakati iliyotumika ilikua mingi ikiwemo kumaliza silabasi mapema na kufanya marudio ya mada mbalimbali pamoja na kuzifanyia mitahani ya ndani na nje.

Kwa upande waka kiranja wa Taaluma wa Shule hiyo, Gratnes Mlashan amesema kuwa matokeo ya Kidato cha Sita wameyapokea vizuri kwa sababu yamewafurahisha na kuwatia moyo kuendelea kufanya vizuri mitihani inayokuja.

“Natoa wito kwa wanafunzi wenzangu kusoma kwa bidii kuhakikisha kuwa matokeo haya hatushuki ispokuwa tupate matokeo zaidi ya haya,” amesisitiza Mlashan

Naye Kiranja Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi katika Shule hiyo, Ernest Munishi amesema kuwa matokeo ya Kidato cha sita yamekuwa ni msingi mkubwa kwao kuhakikisha  wanasoma kwa bidii na kuzingatia maelekezo ya walimu wao ili wafaulu zaidi.

“Ndugu zangu wanafunzi fahamuni kuwa kila kitu kinawezekana kama walivyoweza kufaulu wenzetu, sisi tufaulu zaidi na kuingia kumi bora inawezekana,” ametilia mkazo Munishi

Ufaulu wa Shule ya Sekondari Lulumba umeongezeka kwa Mwaka wa masomo 2020 ukilinganisha na mwaka 2019 ambapo ilishika nafasi ya pili kimkoa na ya kwanza kushikwa na Shule ya Sekondari Mwanamwema

MWISHO

Mkuu wa Shule ya Lulumba Sekondari, Jeremia Kitiku akielezea mikakati iliyowawezesha wanafunzi 151 kufaulu na kuwa yakwanza Mkoa wa Singida ya 23 Kitaifa. Picha na Hemedi Munga

Mwalimu wa Jografia Shule ya Lulumba Sekondari, Daud Noa akielezea mikakati aliyotumia kuifanya Shule hiyo kushika nafasi ya sita kwa Somo la Jografia Kitaifa kati ya Shule 737 na ya kwanza kimkoa. Picha na Hemedi Munga

Kiranja wa Taaluma wa Shule ya Sekondari Lulumba, Gratnes Mlashan akihadi kuwa wanahitaji kuingia kumi bora kitaifa matokeo ya mitihani itakayofuata. Picha na Hemedi Munga

Kiranja Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi, Ernest Munishi akieleza namna matokeo ya kidato cha sita yalivyoamsha ari ya kujisomea na kufuata maelekezo ya walimu wao ili waweze kufaulu zaidi. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.