
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Ndugu Michael Agustino Matomora akipanda mti Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa.
Zoezi la upandaji miti Kimkoa limeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego ikiwa ni Maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Disemba 9.

Jumla ya Miti 501 imepandwa eneo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa kuadhimisha sherehe za Uhuru Mkoani Singida.
Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara: “UONGOZI MADHUBUTI NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI NI MSINGI WA MAENDELEO YETU.”
KIOMBOI, IRAMBA
Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA
Telephone: 026 - 2532253
Mobile: 026 - 2533001
Email: ded.irambadc@singida.go.tz
Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.